Kwa mujibu wa mbunge wa Mbulu vijijini Mhe. Flatei Massay mtu moja ambaye ni mwandishi wa habari amepoteza maisha.
Inasemekana chanzo cha ajali hiyo ni Twiga aliyekuwa anakatisha barabara mbele yao na katika kumkwepa gari likapinduka.
Taarifa zinapasha kuwa Dkt. Kigwangwala amepata majeraha ya mkono na kifua na kukimbizwa katika kituo cha afya cha Magugu kupatiwa matibabu na kwa mujibu wa mleta habari, hali sio nzuri sana.
Hivi sasa inasubiriwa helikopta ije kumchukua kumpeleka hospitali kubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...