Taarifa zilizopatikana muda huu zinasema Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamisi Kigwangwallah  amepata ajali asubuhi hii akitokea Arusha katika eneo la msitu kabla ya kijiji cha Magugu maarufu kama Mguu wa Mjerumani ama Mdori.
Kwa mujibu wa mbunge wa Mbulu vijijini Mhe. Flatei Massay mtu moja ambaye ni mwandishi wa habari amepoteza maisha.  
Inasemekana chanzo cha ajali hiyo ni Twiga aliyekuwa anakatisha barabara mbele yao na katika kumkwepa gari likapinduka.
Taarifa zinapasha kuwa Dkt.  Kigwangwala amepata majeraha ya mkono na kifua na kukimbizwa katika kituo cha afya cha Magugu kupatiwa matibabu na kwa mujibu wa mleta habari, hali sio nzuri sana.
Hivi sasa inasubiriwa helikopta ije kumchukua kumpeleka hospitali kubwa. 
Tunafuatilia kwa karibu tutatoa taarifa zaidi baadaye.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...