Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Bw.Khatib Abdulrahman Khatib Babu mara alipowasili katika ufunguzi wa Jumba la "Chawi" maarufu Jumba la Treni liliopo Dajani Mjini ambalo limefanyiwa matengenezo makubwa na Kampuni ya CRJE kutoka China, wakati wa sherehe iliyofanyika jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto)akifungua pazia kama ishara ya kulifungua Jumba la "Chawi" maarufu Jumba la Treni liliopo Dajani Mjini Zanzibar lililofanyiwa matengenezo makubwa na Kampuni ya CRJE kutoka China, wakati wa sherehe rasmi iliyofanyika leo (kulia) Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Khalid Mohamed Salum.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF Bibi.Sabra Issa Machano (mbele) wakati alipotembelea sehemu mbali mbali za Jengo la "Chawi" maarufu Jumba la Treni lililofanyiwa matengenezo makubwa na Kampuni ya CRJE kutoka China liliopo Dajani Mjini Zanzibar baada ya kulifungua rasmi katika sherehe zilizofanyika jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...