Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akiwasili katika Gereza la Kilimo Mang’ola, Wilayani Karatu Agosti 2, 2018 tayari kwa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua shughuli mbalimbali za uendeshaji wa Jeshi hilo.
 Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Anderson Kamtiaro(wa tatu toka kulia) akimuonesha Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(wa pili kushoto) ramani ya eneo linapojengwa Gereza la jipya la Mahabusu Wilayani Karatu.

 Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akikagua tanuru la tofali za kuchoma katika eneo la Gereza la Kilimo Mang’ola. Tofali hizo za kuchoma hutumika kujenga nyumba za watumishi katika gereza hilo.
 Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akizungumza na Askari wa Gereza Mang’ola(hawapo pichani) katika ziara yake ya kikazi.
 Askari wa vyeo mbalimbali wa Gereza Mang’ola wakifuatilia kwa makini maelekezo ya Kamishna Jenerali wa Magereza.
 Mkuu wa Gereza Mang’ola, Mrakibu wa Magereza, Masesa Magere(wa kwanza kushoto) akimuonesha Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike maeneo mbalimbali ya gereza hilo leo Agosti 2, 2018
Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega(kulia) akiwa ameongezana na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(wa pili kushoto) katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa Arusha. Kamishna Jenerali Kasike amefika Ofisi za Mkuu wa Mkoa Arusha kabla ya kuanza ziara yake katika Gereza la Kilimo Mang’ola leo Agosti 2, 2018
(Picha zote na Kitengo cha Habari na
Mawasiliano Makao Makuu ya  Jeshi la Magereza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...