Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, akihutubia Bodi ya Wakurugenzi, Viongozi na Mameneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara, kuhusu umuhimu wa kusimamia ipasavyo makusanyo ya kodi, katika kikao maalumu kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kilimanjaro wa Benki Kuu ya Tanzania, Jijini Dar es Salaam

 Wajumbe wa Menejimenti wa Wizara ya Fedha na Mipango, wakiwa pamoja na Viongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, kujadili namna ya kuhakikisha kuwa zaidi ya shilingi trilioni 18 kati ya shilingi trilioni 32.47 zilizopitishwa na Bunge kwa ajili ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2018/2019 zinazotakiwa kukusanywa na Mamlaka hiyo zinapatikana kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo.
 Meza Kuu ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (wa tatu kulia), wakati wa kikao maalumu kati ya Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Mipango na Bodi ya Wakurugenzi, Menejimenti ya TRA na Mameneja wa Mamlaka hiyo kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara, waliokutana katika ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu, Jijini Dar es Salaam, kujadili pamoja na mambo mengine namna ya kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Susana Mkapa na Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Adolf Ndunguru.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, akisisitiza jambo kwa Bodi ya Wakurugenzi, Viongozi na Mameneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara, kuhusu umuhimu wa kusimamia ipasavyo makusanyo ya kodi, katika kikao maalumu kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kilimanjaro wa Benki Kuu ya Tanzania, Jijini Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...