Katibu Mkuu  Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi. Susan Mlawi   akizungumza leo Jijini Dodoma na wachezaji walioshiriki mashindano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki  (hawapo katika picha) ambapo timu ya mpira wa miguu wanawake waliibuka washindi wa kwanza, katikati ni Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Harrison Mwakyembe na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuph Singo.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe  akisisitiza jambo kwa wachezaji walioshiriki mashindano ya Jumuiya ya Afrika Masharik (hawapo katika picha), wakati wa halfa ya kuwapongeza wachezaji hao leo Jijini dodoma, kwanza kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Zanzibar Bw.Hamis Alli Mzee,anayefuata ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bibi. Susan Mlawi na  kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuph Singo.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja  na wachezaji wa timu ya Karate.

Katibu Mkuu  Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi. Suzan Mlawi (katikati)  akifurahi pamoja na wachezaji wa mpira wa pete  leo Jijini Dodoma  baada ya timu hiyo kurejea ikitokea Bujumbura nchini Burundi ilipokuwa ikishiriki mashindano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo iliibuka mshindi wa pili.
(Picha na Shamimu Nyaki-WHUSM)

Na Shamimu Nyaki –WHUSM
WAZIRI wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa mwanamichezo anayepaswa kujivunia mafanikio katika michezo ni yule ambaye ameiletea nchi sifa nzuri ya ushindi.

Hayo ameyasema leo Jijini Dodoma katika halfa ya kuzipongeza timu zilizoshiriki mashindano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika mjini Bujumbura nchini Burundi ambapo timu ya mpira wa miguu ya wanawake waliibuka washindi wa kwanza.
 “Sasa naona wachezaji  wetu mmebadili muelekeo kwa kuweka juhudi na kuhakikisha mnailetea heshima nchi yetu kwa kuja na kombe la ushindi, hiki ndio kilele cha mafanikio kwa wanamichezo” alisema Dkt. Mwakyembe.

Anazidi kueleza kuwa  Serikali itaendelea kuweka juhudi kwa timu za wanawake ambazo zimeonyesha mafanikio makubwa katika michezo kwani zimekuwa zikifanya vizuri  ambapo ndani ya muda  wa miezi miwili zimeleta makombe mawili kutoka katika mashindano ya kimataifa ikiwemo  CECAFA.

Dkt. Harrison Mwakyembe alisisitiza kuwa zama za kupeleka wachezaji kwa mazoea zimepitwa na wakati bali wachezaji watakaokuwa wakishiriki michezo ya nje ya nchi ni wale wenye juhudi na uzalendo kwa taifa lao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...