Na Leandra Gabriel, Glogu ya jamii
KITUO cha Sheria na haki za binadamu (LHRC)  kimezindua ripoti ya nusu mwaka ikionesha hali ya haki za binadamu katika kipindi cha miezi 6 ya mwaka 2018 yaani kuanzia Januari hadi Juni.

Akizungumza na wanahabari katika uzinduzi huo Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho na Wakili  Anna Henga ameeleza kuwa ripoti hiyo imeandaliwa kwa kutumia vyanzo mbalimbali kama vile jeshi la polisi, ripoti za mashirika mbalimbali pamoja na vyombo vya habari na ripoti hiyo imegawanyika katika makundi matatu ambayo ni haki za kiraia na kisiasa, haki za kijamii na haki za za makundi maalumu.

Henga ameeleza kuwa ripoti hiyo imeibua mambo muhimu ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa kiasi kikubwa kwa ukatili dhidi ya watoto hasa ukatili wa kingono na ubakaji mara tatu zaidi ukilinganisha na kipindi cha mwaka 2017 na hii ni kwa kulinganisha matukio 12 kwa mwaka 2017 kufikia matukio 533 kwa mwaka 2018 na kati ya matukio 6376 ya ukiukwaji wa haki za watoto  matukio 2365 yametokana na ubakaji na matukio 533 ni ulawiti 

Pia ameeleza kuwa ukatili dhidi ya wanawake umeongezeka  hasa wa kingono na mwili ambapo matukio ya ubakaji yaliyoripotiwa  kuanzia mwezi Januari hadi Juni mwaka huu yamefika1218 ikikadiriwa idadi ya wanawake 203 hubakwa kwa mwezi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...