Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii
WAKILI wa Kujitegemea Leonard Manyama amesema kuwa serikali ya awamu ya Tano chini ya Dk.John Pombe Magufuli itawavusha watanzania kwenda katika uchumi wa maendeleo wa kufanya kazi pamoja na ulipaji wa kodi.

Manyama aliyasema hayo wakati aliposhuka katika uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akitokea nchini Marekani amesema amejifunza vitu vingi nchini Marekani ambavyo ndivyo Rais Dk.John Pombe Magufuli anapigania katika watu kufanya kazi pamoja na ulipaji wa kodi.

Amesema kuwa ulipaji wa kodi nchini Marekani ni sheria na hakuna majadiliano juu ya ulipaji wa kodi ambapo ndicho kinachofanyika sasa.

Manyama amesema maendeleo yatapatikana tu ikiwa kila mtu atafanya kazi pamoja na kulipa kodi ambayo ndio itafanya maendeleo ya kufikia uchumi wa kati.

Aidha amesema kuwa nchi hii imejaliwa rasimali za kutosha ambazo Rais anazipigania hivyo kila mtu kumuunga mkono kwa vitendo katika kufanya kazi na kusimamia rasilimali zilizopo.

“Nina imani ya Rais kuwa nilichoona nchini Marekani ndicho kinafanyika kwetu katika kuhakikisha kila mtu analipa kodi ambayo sasa indio itafanya mapinduzi katika uchumi wa kati katika uboreshaji wa miundombinu ya barabara , Afya na Mambo mengine mbalimbali”amesema Manyama.
Wakili wa Kujitegemea Leonard Manyama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo mara baada kuwasilia katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akitokea nchini Marekani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...