Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde leo ametimiza ahadi ya kumpatia Kijana Dominic Oscar Mbele Mwanachuo wa Chuo kikuu cha Dodoma pikipiki ya matairi matatu (bajaj) ili kumsaidia kuyafikia maeneo mbalimbali kwa haraka na kwa urahisi.

Bajaj hiyo imekabidhiwa leo na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Wenye Ulemavu) Mh Stella Ikupa ambaye amemshukuru Mh Mavunde na wote waliochangia kwa moyo wao wote na kutoa rai kwa jamii kusaidia watu wenye ulemavu badala ya kuliachia jukumu hilo serikali na viongozi peke yako.

Akishukuru baada ya kukabidhiwa Bajaj hiyo Ndg Dominic Mbele ambaye ni Mwanachuo wa Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) anayesomea Shahada ya Kwanza ya masuala ya Kompyuta amemshukuru sana Mh Mavunde na wote waliomchangia kwa moyo wa kipekee wa kumsaidia kupata usafiri huo na kuahidi kuwaombea kwa Mungu ili Mungu awazidishie.
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde akimkabidhi kijana Dominic Oscar Mbele ambaye ni Mwanachuo wa Chuo kikuu cha Dodoma pikipiki ya matairi matatu (bajaj) ili imsaidie kuyafikia maeneo mbalimbali kwa haraka na kwa urahisi.
kijana Dominic Oscar Mbele ambaye ni Mwanachuo wa Chuo kikuu cha Dodoma akimshukuru Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde kwa kumpatia pikipiki ya matairi matatu (bajaj) ili imsaidie kuyafikia maeneo mbalimbali kwa haraka na kwa urahisi.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Wenye Ulemavu) Mh Stella Ikupa akimpa mkono wa pongezi kijana Dominic Oscar Mbele ambaye ni Mwanachuo wa Chuo kikuu cha Dodoma kwa kufanikiwa kuipata baiskeli hiyo (bajaj) ,iliyotolewa na Mh Mavunde.Aidha Mh Ikupa  rai kwa jamii kusaidia watu wenye ulemavu badala ya kuliachia jukumu hilo serikali na viongozi peke yako.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...