Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

MBUNGE wa jimbo la Mtama Nape Nnauye amewataka Wapinzani kuja kubishana kwa hoja mambo gani waliyoyafanya katika jimbo la Buyungu na CCM waliyoyafanya kuwaletea miradi ya maendeleo Wananchi wa Buyungu na sio kuwadanganya Wananchi wa Buyungu.

Pia amesema Upinzani wasipobadilika siasa Wanazozifanya kwa sasa upinzani utafutika kwa kuwa Wananchi wanaona kazi inayofanywa na serikali iliyoko madarakani na wasipo badiliku na kuacha kuisema vibaya Watakimbiwa na Viongozi wote na wanachama.

Nnauye amesema hayo leo katika kijiji cha Nyakayenzi kata ya Kasuga,Wilayani kakonko wakati akimnadi mgombea wa chama hicho, ambapo alisema wapinzani wanatakiwa kubishana kwa hoja kwa kutangaza mazuri waliyoyafanya kwa kipindi cha miaka mitatu waliyoaminiwa na wananchi wa Buyungu,  ni miradi ipi walioileta na vitu walivyovifanya.

Amesema nje ya miradi iliyotekelezwa na serikali ya chama cha mapinduzi wakati wa utawala wa mgombea ambae anagombea kiti hicho hakuna ambacho walikifanya Chadema, na wanatakiwa kuacha kuwadanganya wananchi kwamba wao wamefanya kwakuwa hawana serikali na serikali iliyopo madarakani ni ya CCM.

Amesema kwa kipindi ambacho Christopher Chiza amekuwa madarakani ameweza kuleta miradi ya kilimo cha mpunga katika skimu za umwagiliaji za Katengera na Ruhiti pamoja na umeme na miradi ya maji ambapo amewaomba Wananchi wamchague Chiza aweze kuendeleza miradi ambayo haijakamilika.
 MBUNGE wa jimbo la Mtama Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa 
kijiji cha Nyakayenzi kata ya Kasuga,Wilayani kakonko wakati akimnadi mgombea Ubunge wa chama hicho Ndugu Christopher Chiza
Baadhi ya Wananchi na wafuasi wa chama cha Mapinduzi wakifuatilia mkutano wa kampeni ,wakati Mbunge wa jimbo la Mtama Nape Nnauye alipokuwa akimnadi mgombea Ubunge wa chama hicho Ndugu Christopher Chiza katika kijiji cha Nyakayenzi kata ya Kasuga,Wilayani kakonko mkoani Kigoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...