MKUU wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Kawawa amewataka vijana ambao wanahitimu mafunzo ya jeshi la akiba kuhakikisha wanakuwa wazalendo na nchi yao na kuachana kabisa na vitendo vya kujiingiza katika matukio ya kihalifu na badala yake wahakikishe wanazingatia sheria na taratibu zote zilizowekwa kwa lengo la kuweza kulinda hali ya ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao. 
 Kauli hiyo ameitoa wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa mafunzo ya awali ya jeshi la akiba ambayo yamefanyika katika kata ya Bwilingu na kuwajumusiha vipana wapatao 183 kutoka katika halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani. 
 Mkuu huyo pia amewahimiza vijana hao kuhakikisha wanakuwa na nidhamu ya hali ya juu katika kipindi chote cha mafunzo hayo ya kijeshi na kuzingatia maelekezo ambayo wanapatiwa na walimu wao kwa lengo la kuweza kujifunza mbinu mbali mbali ambazo zitaweza kuwa ni mkombozi mkubwa katika kulilinda Taifa la Tanzania na kuweza kukabiliana na wimbi la matukio ya uhalifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...