Tumaini Mikindo Mkurugenzi mtendaji wa PANITA akitoa salamu kwa niaba ya Asasi za Kiraia kwa Waziri Jaffo wakati wa kikao hicho
Picha ya pamoja na Makatibu tawala waliohudhulia kikao
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii.
SERIKALI kupitia Halmashauri imeshauriwa kujenga tabia ya kutenga fedha kupitia mapato yao ya ndani ili kuweka mfumo thabiti na endelevu katika kuboresha hali ya lishe na ambao utajengeka juu ya msingi bora unaowekwa na fedha za wafadhili pindi miradi hii itakapokwisha.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa PANITA Tumaini Mikindo kwa niaba ya Asasi za kiraia ambazo zimejikita katika masuala ya lishe nchini wakati wa kikao kati ya na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) Suleiman Jaffo.
Lengo la kikao hicho kimekutana kwa ajili ya kuifanya tathimini taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa lishe baina ya Makamu wa Rais, Wakuu wa Mikoa wa Tanzania Bara na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali.
Hivyo Mikindo ameshauri ni vema pia halmashauri ziweke vipaumbele kwenye afua za lishe ambazo zitaleta matokeo chanya kwa haraka. Pia Serikali iongeze bajeti ya lishe kutoka Sh.1,000 ya sasa kwa mtoto hadi kufikia Sh. 23,000 ambayo ni takribani dola 8.5 za kimarekani kwa mwaka kwa kila mtoto chini ya miaka mitano na iwapo wanalenga kufikia maazimio ya Baraza la Afya Duniani (WHA) kuhusu lishe kufikia 2025.
"Baada ya maneno haya machache namshukuru Waziri Jafo kwa kutushirikisha katika kikao hiki adhimu cha kujadili utekelezaji wa mkataba wa lishe,"amesema Mikindo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa leo kuhusu kikao hicho cha tathimini.
Awali wakati anaanza kuzungumza Mikindo amesema asasi za kiraia zinatoa shukrani kwa Waziri Jaffo kwa kuwaalika kwenye mkutano huo na kwao ni fursa ya kutoa maoni yao kuhusu lishe nchini.
"Hii ni uthibitisho tosha Serikali ya Awamu ya tano chini ya Rais Dk.John Magufuli inavyothamini na kutambua mchango wa wadau ikiwemo Asasi za kiraia katika kusukuma gurudumu la maendeleo ya taifa hili kuelekea uchumi wa kati kupitia viwanda ifikapo 2025.Waziri tunaomba utufikishie shukurani zetu za dhati kwa Rais,"amesema.
Aidha amesema wanamshukuru Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kwanza kwa kukubali kuwa kinara wa lishe na pili kwa kutimiza ahadi aliyoitoa siku ya uzinduzi wa ripoti ya lishe ya dunia nchini Tanzania Julai 20 mwaka 2016 jijini Dar es Salaam.
"Naomba nirejee baadhi ya maneno aliyoyatamka siku hiyo. Ninanukuu, “…Ni kweli kwamba kwenye “Political will” jambo lolote linaweza likafanyika; kwa hiyo niseme kwamba na hili suala la lishe tutalipa msukumo mkubwa wa kisiasa ili kila mmoja wetu aimbe lishe na kupunguza Utapiamlo,"amesema wakati anatoa nukuu hiyo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...