Na Gaudensia Simwanza – Urambo.

TFDA kwa kushirikiana na uongozi wa Wilaya ya Urambo, mkoani Tabora, wanaendesha mafunzo ya siku tano kwa wajasiriamali wadogo 150 wa usindikaji wa vyakula wilayani humo kuanzia leo tarehe 20/8/2018  ili kuchangia  ukuaji wa Sekta ya viwanda nchini sanjari na kuinua uchumi wa wananchi wa Urambo.

Mafunzo hayo yamefunguliwa na Mgeni Rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Angelina Kwingwa na kuhudhuriwa na viongozi wengine wa Wilaya hiyo wakiwemo Mbunge,  Mhe. Margareth Sitta (Mb.), Katibu wa CCM wa wilaya, Bi. Jesca Mbogo na Mkurugenzi wa wilaya, Bi. Margareth Nakainga miongoni mwa viongozi wengine.

”TFDA inatambua mchango mlio nao katika kukuza viwanda vidogo vya chakula kwani kutokana na uwingi wake vina mchango mkubwa katika; kuongeza ajira na kipato katika ngazi ya kaya, kukuza kilimo cha mazao ya chakula na kuyasindika na hatimaye kuiwezesha Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda na ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025”, alisisitiza Mgeni Rasmi huyo.

Ili kuwawezesha wajasiriamali wadogo nchini kutatua changamoto zinazowakabili katika usajili wa majengo na bidhaa zao, uongozi wa Wilaya umeamua kuweka mkakati wa makusudi ikiwa ni pamoja na kuwaalika wataalam wa Serikali kuja kutoa mafunzo kama haya ili kuinua maisha ya wananchi wake na Taifa kwa ujumla”, Mkuu huyo wa Wilaya aliongeza.

TFDA inaendelea kushirikiana uongozi wa Mikoa na Halmashauri zake ili kuwawezesha Watanzania kuanzisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa kwa kuzingatia vigezo vya usalama na ubora ili kupata soko la ndani na nje ya nchi kwa bidhaa zetu kwa maendeleo ya Taifa
 Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Angelina Kwingwa, (aliyesimama) akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mafunzo yanayoendeshwa na TFDA kwa Wajasiriamali wa Wilaya ya Urambo. Viongozi wengine wa wilaya hiyo kutoka kushoto ni Mbunge wa wilaya Mhe. Margareth Sitta (wa tano), Mkurugenzi wa wilaya, Bi. Margareth Nakainga (wa sita), Meneja wa TFDA Kanda ya Magharibi, Dkt. Edgar Mahundi (wa saba), Katibu wa (CCM) wa wilaya, Bi. Jesca Mbogo (wa tatu), na Mwenyekiti wa semina hiyo, Bi. Martha Susu (wa n ne).
 Mbunge wa wilaya ya Urambo Mhe. Margareth Sitta (aliyesimama), akiwasalimia wajasiriamali wanaohudhuria mafunzo wilayani Urambo.
Sehemu ya Wajasiriamali  wilaya ya Urambo wakifuatilia mafunzo yanayotolewa na (TFDA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...