Na.Vero Ignatus -Arusha 

Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania inaendelea kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji juu ya uthibiti wa viasilia vya mionzi vinavyoweza kupatikana kwenye mazao ya chakula na mifugo ili kuongeza usalama wa mtumiaji dhidi ya madhara hatari yanayosababishwa na mionzi.

Katika maonyesho ya nanenane kanda ya kaskazini wanatoa elimu juu ya nyuklia inayoweza kuwa mkombozi kwenye ukuaji wa uchumi wa biashara na viwanda ikilenga matumizi salama teknolojia nchini ili kuboresha ustawi wa kwenye sekta ya afya,maji ,kilimo,nishati na mifugo.

Mtafiti wa Tume ya Nguvu ya Atomiki Yesaya Sungita amesema takwimu zinaonyesha kwamba zaidi ya asilimia 30%ya vyakula duniani vinahribika kila mwaka kwa sababu ya kuharibiwa na na vijidudu au kuoza ,upotevu au kuharibika kwa chakula kuna athari kubwa katika kipato cha wakulima.

Aidha kila mwaka inakadiriwa hasara inayotokana na kuharibika kwa mazao ya nafaka barani Afrika haswa kusini mwa jingo la sahara inafikia dola za kimarekani bilioni 4 sawa na asilimia 15 ya thamani ya mavuno hayosambamba na matukio ya binadamu kuambukizwa vijidudu vya salmonella yanafikia iddi ya watu 120,000 kila mwaka ambapo maambukizi yamekuwa yakisbabisha vifo vingi.

"Gharama ya matibabu yanayosababishwa na madhara ya maambukizi haya ya vijidudu vya salmonella na Ecoli yamekuwa yakisababisha hasara ya dola za kimarekani bilioni 6 kila mwaka.alisema Yesaya" 
Kutoka kulia ni Mtafiti kutoka Tume ya Nguvu za Atomiki Yesaye Sungita, wa  kwanza kushoto ni Afisa Mawasiliano wa Tume Peter Ngamilo akiguatiwa na  Mtafiti wa Tume hiyo Jerome Mwimanzi wakitoa elimu kwa mmoja wa mgeni  aliyetembelea katika banda hilo katika maonyesho ya nane nane Kanda ya Kaskazini katika viwanja vya Themi Njiro Arusha. 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...