Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

SERIKALI imesema kuwa wenye viwanda vya saruji wazalishe saruji ya kutosheleza mahitaji ya ndani pamoja na kusimamia bei ya bidhaa hiyo mpaka kwa mlaji wa mwisho.

Hayo ameyasema Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charle’s Mwijage wakati alipotembelea viwanda vya Saruji vya Camel na Twiga , amesema amekosa hivi usingizi kwa kuadimika kwa saruji nchini na kuwataka viwanda hivyo vizalishe saruji ya kukidhi mahitaji ya ndani kutokana na kuwepo miradi mbalimbali ya ujenzi.

Mwijage amesema kuwa hivi karibuni kulikuwa kuadimika kwa saruji iliyotokana na baadhi ya viwanda kuwa katika matengenezo pamoja na makaa ya mawe kuzalishwa kwa kiwango kidogo.Amesema kuwa katika kusimamia wizara hiyo kwa mzalishaji ambaye hatakwenda na kasi ya uzalishaji wa saruji anatomlaka ya kuifuta leseni hivyo wenye viwanda lazima wakidhi mahitaji ya saruji.

Aidha amesema kuwa kwa mwaka tani milioni 10.5 zinalishwa hivyo lazima kila kiwanda kiongeze uzalishaji na kuweza kuuza hata masoko ya nje ya nchi kwa kupata fedha za kigeni zinazotokana na saruji.Amesema kuwa kuna viwanda vitatu vya saruji vinajengwa nchini ambavyo vitaongeza uzalishaji wa wa saruji hiyo.

Mwijage amesema kuwa viwanda vikizasha saruji na kuweza kuuza katika masoko ya nje kuna uwezekano wa bidhaa ya saruji ikwa inachangia uchumi wa nchi na kuongoza katika uchangiaji huo kwa pato la taifa.Meneja wa Masoko wa kiwanda cha Saruji cha Twiga , Danford Semwenda amesema kuwa kwa sasa wanazalisha tani 6000 kutoka tani 300O kwa siku 15 zilizopita iliyotokana na matengenezo ya mtambo.

Waziri Mwijage leo Augusti 27,2018 ametembelea viwanda vya kutengeneza Saruji kuanzia cha Camel kilichopo Mbagala rangi Tatu na cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akitembelea kiwanda cha Camel kilichopo Mbagala jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuangalia utendaji kazi wa kiwanda hicho kutokana na kukosekana kwa saruji hapa nchini.
  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akitembelea kiwanda cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaam na kushoto ni Mkurugenzi Mkuuwa Kiwanda cha Twiga, Alphonso Velez.
 Mchanga wa kutengeneza Saruji katika kiwanda cha Saruji cha Twiga Tegeta jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Masoko wa kiwanda cha Saruji cha Twiga , Danford Semwenda akijibu swali kutoka kwa  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alipotembelea kiwanda cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mkurugenzi Mkuuwa kiwanda cha Twiga kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaa, Alfonso Velez.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...