Na Bashiri Salum- Dodoma
Uwepo wa tija ndogo katika Sekta ya kilimo na taknolojia chache hapa nchini kumetokana na
kutengewa kiasi kidogo cha fedha kutoka serikalini na kwa wadau wa maendeleo.
Hayo yamesemwa na kaimu mtendaji mkuu wa taasisi ya Utafiti wa Kilimo TARI Dkt Degratius
Rwezaura ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano uliowakutanisha watafiti wa kilimo na
mifugo uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa wakala wa uhifadhi wa chakula
wa taifa NFRA uliopo Dodoma.
Dkt Rwezaura amesema kwamba fedha zinzotengwa na serikali kwa ajili kufanya utafiti wa
kilimo zimekuwa ndogo hivyo kushindwa kukamilisha lengo la watafiti kubuni teknolojia
mbaliambali za kilimo na mifugo ambazo ni muhimu sana katika kipindi hiki cha uchumi
viwanda.
Aidha Dkt Rwezaura amesema utafiti wa kilimo na mifugo hapa nchini umekuwa ukigharimu
kiasi kikubwa cha fedha kwakuwa uwekezaji katika miundombinu ya utafiti ikiwemo ujenzi wa
vyumba vya baridi vya kuhifadhi mbegu(cold room) na mahabara za kutosha haujafanyika
kikamilifu hivyo kulazimu kuendelea kuhifadhi mbegu katika vitalu kwa kulilima kila mwaka.
“Kama tungekuwa na mahabara jini tungeweza kuifadhi na kusambaza mbegu bora za kilimo
na mifugo kwa wakati badala ya kulima kwenye vitalu kila mwaka ili kuepuka kuharibika kwa
mbegu.” Allisema Dkt. Rwezaura
Hata hivyo amebainisha kwamba takwimu zinaonesha kuwa Serikali imenachangia asilimia 0.17
katika uwekezaji kwenye utafiti ikilinganishwa na nchi nyingine kama Uganda na Kenya ambazo
katika utafiti wamewekezeza asilimia 4.6 alisema Dkt. Rwezaura
“Kilimo chetu kimeendelea kukosa tija kwa sababu ya uwekezaji mdogo wa fedha kutoka kwa
wafadhili na serikali ”alisistiza Dkt Rwezaura
Aidha Dkt. Rwezaura alimalizia kwa kusema kwamba lengo la mkutano huo ni kutengeneza
hoja na kukutana na watunga sera ili kuweza kutafuta fedha za kuendeleza utafiti wa kilimo na
mifugo kwa ajili ya upatikanaji wa malighafi za viwandani.
Naye Dkt Bakari Msangi kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia ( COSTECH) amesema
kwamba Taasisi hiyo imeratibu tafiti nyingi hapa nchini kupitia mfuko wa serikali hasa katika
sekta ya kilimo mifugo na uvuvi lengo likiwa ni kurahisisha ufanywaji wa tafiti mbalimbali.
Aidha Dkt Msangi amebainisha kwamba watafifi wapatao 517 walijengewa uwezo kupitia Tume
ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia katika kiwango cha uzamili na uzamivu lengo ni kuwafanya
waweze kuimarisha sekta ya kilimo
Hata hivyo Dkt Msangi amesisitiza kwamba kuanzia mwaka 2010-16 wameweza kupeleka kiasi
cha shilingi bilioni 5. 1 kwa watafiti kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya utafiti ikiwemo
ujenzi wa mahabara katika maeneo ya Zanzibari,makutopora Dodoma, Mpwapwa Naliendele na
katika Mikoa ya wa Kilimanjaro.
Amesema COSTECH wamekuwa wakiratibu ujenzi wa miundombinu ya utafiti kwa sababu ya
umuhimu mkubwa wa mazingira bora katika ufanyaji wa utafiti
Aidha ametoa wito kwa watafiti kufanya tafiti zenye ubunifu ili kuendana na mahitaji na
kuwafikiwa walengwa kwa wakati.
utafi kwa sasa unatakiwa kwenda na ubunifu kwa sababu mazao ya utati yapo mengi lakini
haziendi mara kwa watumiaji kutokana na kutotumika kwa ubunifu wa kutosha hivyo kwa sasa
tunasisitiza sana ubunifu kwenye tafiti ili ziweze kuwavutia walengwa. Alisema Dkt Msangi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...