Ikiwa imepita miezi miwili tangu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola kuagiza pikipiki zote zinazotumika kusafirisha abiria zifungwe tela katika kile kinachoaminika kudhibiti wimbi la ajali za bodaboda,Taasisi mbalimbali za Serikali zimekutana jijini Dodoma ikiwa ni mazungumzo ya awali kuelekea mkakati huo wa kupunguza ajali.

Akizungumza jijini Dodoma baada ya mkutano na ukaguzi wa pikipiki ya mfano iliyofungwa tela iliyotengenezwa na Shirika la Mzinga,lililoko chini ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, amesema Serikali imedhamiria kuondoa na kukomesha ajali za bodaboda pamoja na kulinda usalama wa watumiaji wa usafiri huo.

Akielzezea juu ya mazungumzo hayo yaliyokutanisha taasisi hizo, Katibu Mkuu Meja Jenerali Jacob Kingu, amesema Wizara yake kwa kushirikiana na wadau wengine kutoka taasisi za serikali; Shirika la Mzinga, Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Kiwanda cha Kutengeneza Magari (NYUMBU) na Jeshi la Polisi watahakikisha wanakuwa na mpango wa pamoja wa kuratibu na kuhakikisha mkakati huo utakaosaidia kupunguza ajali unakamilika.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akiwa amepanda Pikipiki ya mfano iliyotengenezwa na Shirika la Mzinga, lililoko chini ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ikiwa ni hatua za awali katika utekelezaji wa agizo la Serikali ili kukabiliana na ajali za bodaboda pamoja na usalama wa watumiaji wa chombo hicho cha usafiri. Tukio hilo limefanyika leo, jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akiwa amepanda Pikipiki ya mfano iliyotengenezwa na Shirika la Mzinga, lililoko chini ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ikiwa ni hatua za awali katika utekelezaji wa agizo la Serikali ili kukabiliana na ajali za bodaboda pamoja na usalama wa watumiaji wa chombo hicho cha usafiri. Tukio hilo limefanyika leo, jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu(aliyepanda pikipiki), akisikiliza maelezo ya kiufundi kutoka kwa mmoja wa wataalamu kutoka Shirika la Mzinga, Whemy Lyimo(kulia) waliotengeneza pikipiki hiyo yenye tela ikiwa ni hatua za awali katika utekelezaji wa agizo la Serikali ili kukabiliana na ajali za bodaboda pamoja na usalama wa watumiaji wa chombo hicho cha usafiri, Kushoto ni dereva wa pikipiki hiyo,Stanley MsuyaTukio hilo limefanyika leo, jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akizungumza na timu ya wataalamu kutoka Taasisi za Serikali baada ya kukagua Pikipiki ya mfano iliyotengenezwa na Shirika la Mzinga, lililoko chini ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ikiwa ni hatua za awali katika utekelezaji wa agizo la Serikali ili kukabiliana na ajali za bodaboda pamoja na usalama wa watumiaji wa chombo hicho cha usafiri. Tukio hilo limefanyika leo, jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...