Muwakilishi wa wadau wa BancABC Mr. Michael Wilkerson, akizungumza na wateja pamoja na wadau wa BancABC wakati wa mkutano uliofanyika katika hoteli ya Serena Dar es Salaam. Mkutano huo ulikuwa mahususi kwa ajili ya kusisitiza juu ya ahadi ya BancABC kuendelea kutoa na kutengeneza bidhaa bora kwa ajili ya wateja wake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Atlas Mara Group Mr. John Staley akiongea na wateja, wadau na wafanyakazi wakati wa hafla iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam hivi karibuni, kwa lengo la kusisitiza ahadi ya kuendelea kutoa bidhaa za kipekee haswa kwa “retail banking” ambayo anajivunia uzoefu wake. Stejini ni muwakilishi wa wanahisa Mr. Michael Wilkerson, Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa BancABC Mr. Imani John.
Wateja wa BancABC walipowasili kwa ajili ya hafla. Hafla hii iliwaleta pamoja wadau, wateja, uongozi pamoja na wafanyakazi wa benki.
Katika picha ya pamoja, toka kulia Mkurugenzi mtendaji wa Atlas Mara Group Mr John Staley, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa BancABC Mr. Imani John pamoja na muwakilishi wa wanahisa wa BancABC Mr. Michael Wilkerson
Wafanyakazi wa BancABC katika picha ya pamoja baada ya hafla yenye mafanikio iliyoandaliwa na BancABC
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...