JOSEPH MPANGALA, MTWARA      
Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA imetoa mafunzio kwa Wafanyabiashara wa Mkaoni Mtwara kuhusiana na Msamaha wa Riba na adhabu ya malimbikizo ya Madeni ya kodi kwa lengo la kuwawezesha wafanyabishara hao kuweza kutambua masuala yanayohusu Kodi pamoja na kuwahi Kuomba Msamaha wa Riba na Adhabu zake.
Akifungua mafunzo hayo kwa Niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evod Mmanda,Katibu Tawala Msaidizi  wa Mkoa wa Mtwara  Renatus Mongogwela amesema katika kipindi kirefu walipakodi wengi walikuwa wanashindwa kulipa Kodi zao kikamilifu kutokana na kuelemewa na malimbikizo makubwa ya Madeni yaliyotokana na Riba na Adhabu.
“Nipende Kuwafahamisha Kuwa Serikali imesikia kilio cha Walipa kodi na kuweka taratibu maalim wa kuyaondoa hayo malimbikizo ya madeni ya riba,hivyo niwasihi ndugu zangu tutumie fursa hii adhim kuweka sawa masuala yenu ya kikodi na kupitia Msamaha huu Serikali inaaamini walipa kodi wataanza upya kuzifuata na kuzitii Sheria hizi”amesema Mongogwela.
Mafunzo hayo ya Siku moja yamejumuisha mabadiliko ya Sheria ya kodi ya  mwaka 2018 pamoja na mfumo wa maadili wa watumishi wa mamlaka ya Mapato Tanzania {TRA} kwa lengo la kuwawezesha wafanyabiashara  kuweza kutoa maoni na kapata huduma Bora.
 Katibu Tawala Msaidi wa Mkoa wa Mtwara Renatus Mongogwela akifungua mafunzo yaliyoandaliwa na mamlaka ya mapato Tanzania {TRA} juu ya elimu ya Msamaha wa riba na adhabu kwa wanyabishara wa Mkoa wa Mtwara.
 Afisa maadili mwandamizi Mika Kiremera  kutoka mamlaka ya mapato Tanzania {TRA}makao makuu akiwasilisha mada kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi pamoja na maadili kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Mtwaa.
 Msimamizi wa Shule ya Sekondari Aquinas Sister Paula Ngagani akiongea na Afisa Mkuu wa elimkwa Mlipa Kodu Makao Mkauu  Julius Ceasar  pamoja na Meneja wa Mamlaka ya mapato mkoa wa Mtwara  Naomi Mwaipola mara baada ya kumalizika kwa mafunzo ya TRA kwa Wafanyabiashara Mkoa wa Mtwara.
 Baadhi ya wafanyabishara waliohudhuria Mafunzo yaliyoandaliwa na Mamlaka ya mapato Tanzania {TRA}Mkoani Mtwara kwa lengo la kutoa elim ya msamaha wa riba na adhabu ya malimbikizo ya madeni ya Kodi,mabadiliko ya sheria ya kodi ya mwaka2018 pamoja na Maadili.
 Wafanyabishara Mkoa wa Mtwara wakiwa pamoja na maafisa wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA mara baada ya Kumalizika kwa mafunzo ya siku moja kuhusina na elimu ya Msamaha wa Riba na adhabu pamoja na maadili kwa watumishi wa TRA>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...