Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MSANII wa Muziki wa Kizazi kipya nchini Bernard Paul 'Ben Pol' ameachia wimbo mpya unaoitwa Ntala Nawe ukiwa  umetengenezwa nchini Kenya chini ya mtayarishaji Cedo. 

 Akizungumza Dar es Salaam, Ben Pol alisema kuwa wimbo huo umetoka kwa Audio na Video ambayo imefanywa hapa nchini na mtayarishaji Hanscana, huku msanii wa filamu Monalisa akiwa muongozaji wake.

 Alisema kuwa tayari Ntala nawe imeshaingia mtaani kwa kusambaza katika vituo mbali mbali vya Televisheni na Radio.

"Mashabiki wangu nimekuja tena na wimbo mpya unaitwa Ntala Nawe naamini mnaoupokea na kuupenda kama nyingine zilizopita, tayari upo YouTube kwa wale wanaopenda kuangalia video na kusikiliza"alisema Ben Pol.. 

 Alisema katika wimbo huo amemshirikisha Cedo kutoka nchini Kenya,  na kwa sasa Ben Pol amekuwa akitamba kwa nyimbo mbalimbali ikiwepo Sofia, Phone, Samboira, Lau nipe nafasi, Gusa na Bado Kidogo pamoja na wimbo wa Amen alioshirikiana na mwanadada Maua Sama.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...