Na Robert Hokororo, Kishapu.

Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu imejipanga kufanya vizuri katika ukusanyaji mapato ili kufikia malengo ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

Hayo yamebainishwa leo Septemba 14, 2018 na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Boniphace Butondo wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani cha kujadili taarifa za robo ya nne ya mwaka 2017/2018.

Alisema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kupitia kwa wataalamu wake imeweka mikakati thabiti kuhakikisha inafika maeneo yote na kukusanya mapato kutoka vyanzo vyake mbalimbali.

“Zipo dalili za kufanya vizuri katika ukusanyaji katika mwaka huu mpya wa fedha ingawa bado kuna changamoto nyingi zinatukabili nawaomba wataalamu msikate tamaa tuendelee kuchapa kazi ili tuwahudumie wananchi,” alisisitiza.

Mhe. Butondo ambaye pia ni diwani wa kata ya Lagana aliwataka madiwani kuendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo zikiwemo ujenzi wa miundombinu mbalimbali.

Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu iliweza kukusanya kiasi cha sh. Bilioni 25.1 kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. Bonophace Butondo akifungua kikao cha Baraza la Madiwani la kujadili taarifa za robo ya nne ya mwaka wa fedha 2017/2018.
Wajumbe wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...