Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 
MKUU wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema amesema kuanzishwa kwa maabara ya sayansi kwa ngazi ya shule za msingi kutasaidia upatikanaji wa wataalamu wa fani hiyo nchini badala ya wataalamu hao kutokana nje ya nchi. 


Mjema amesema hayo jijini Dar es salaam Septemba 22 wakati wa akiweka  jiwe la msingi la ujenzi wa maabara ya kompyuta, ukumbi na mkataba ya shule katika shule ya msingi na awali Queen's pamoja na mahafali ya nane kwa wanafunzi wa awali na darasa la saba. 

Amesema si Mara nyingi sana shule za awali na msingi wakawa na maabara watoto wanaanza wakiwa wachanga watakapofika sekondari watakua wazuri sana ukizingati tuko katika serikali ya uchumi wa viwanda. 

" Tunaanza kuwajenga watoto sasa hivi sisi tunataka kama serikali wataalamu hawa watakua Wahandisi na marubani ambao watatumika maeneo mbalimbali ya viwanda watatoka hapa hapa nchini na hatutaweza kuwategemea wataalamu kutokana nje ya nchi waje hapa" amesema Mjema. 

Aidha ameongeza kuwa wao kama serikali wameunga mkono jitihada hiyo, hivyo shule nyingi zitaanza kuiga mfano wa shule ya msingi ya Queen's ya kuwa na maabara kwa ngazi ya awali na serikali wanampango wa kuanzisha programu hiyo. 

" Serikali tuna mipango mingi tukipata wadau kama nyinyi ambao mtatusaidia hilo litakua jambo pekee sana kwetu" ameongeza Bi Mjema. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shule ya Msingi na awali Queen's Bi Lilian wasira amesema wako hawako kibiashara, shule ipo kwa akili ya kuendeleza elimu kwa jamii wanataka kutengeneza kizazi cha taifa la kesho 

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza katika mahafali ya Nane katika Shule ya Msingi na Awali ya Queen’s iliyopo Ukonga Tabata jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Shule ya Msingi na Awali ya Queen’s Anna Mwalongo akizungumza kuhusiana na shule hiyo kufanya vizuri katika matokeo kwa wanafunzi wanaosoma hapo. 
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akikata Keki kwa ajili ya wahitimu na wazazi katika shule ya Queen’s.

 Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Queen’s Samweli Mwakipesile akizungumza kuhusiana na ujenzi wa Ghorofa kwa ajili ya mabara ya komputa katika shule hiyo.
 Wanafunzi wa Shule ya Queen’s wakitupwiza katika mahafali ya Nane ya Shule hiyo. 
Mkurugenzi wa Shule ya Queen’s Lilian Wassira akiwa amenyanyua mkono kwa ajili ya kuwashukuru walimu wa shule hiyo katika picha hiyo ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...