Na EmanuelMadafa, Globu ya Jamii , Mbeya

WATU 15 wamefariki dunia na wengine 15 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari matano ikiwemo gari dogo la abiria aina Hiace katika eneo la mteremko wa mlima Igawilo Kasoko Nje kidogo mwa Jiji la Mbeya.

Akizungumza Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Nyanda za Juu kusini Mbeya, Petro Siame, alisema hospitali hiyo jana ilipokea miili ya marehemu 13 na majeruhi 15 ambao kati yao wanne walitibiwa na kuruhusiwa.

Siame amesema kuwa alisema, kuwa majeruhi wawili walipoteza maisha wakati wakipatiwa matibabu hivyo idadi ya vifo kuongezeka na kufikia 15 ambapo miili ya watu 12 imetambulika.

‘Jana tulipokea miili ya watu 13 na majeuri 15 lakini kati ya hao wanne wamepatiwa matibabu lakini wawili wamefariki wakati wakiendelea na matibabu hivyo kufanya vifo kuwa 15 na mmoja yupo chumba cha wagonjwa mahututi ICU” alisema Siame

Amesema, majeruhi ambao wanaendelea kupata matibabu wengi wao wamepata majeraha makubwa vichwani na kuvunjika kwa mifupa ya viungo mbalimbali vya mwili ikiwemo mikono na miguu.

Naye Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, akizungumza mara baada ya kuwatembea majehurui waliolazwa katika Hospital ya Rufaa alisema watu 15 kupoteza maisha ni tukio kubwa sana tena kwa ajali ya aina ile ile licha ya serikali kuendelea kutafuta ufumbuzi wa changamoto hiyo.
Mashuhuda wa ajali ya barabarani iliyohusisha magari manne katika eneo la Mteremko wa Igawilo wakitazama moja ya Roli lililopata ajali katika eneo hilo la tukio.
Muuguzi Mkuu Hospital ya Rufaa Kanda ya Mbeya Petro Seme akizungumzia taarifa ya Majeruhi wa ajali.
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (Sugu) akimpa pole mmoja wa madereva wa malori kampuni ya (Asasi) Sabu Mohamed ambaye amelazwa katika hospital ya rufaa Mbeya anako patiwa matibabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...