Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, inatoa pole kwa familia zote ambazo zimepoteza ndugu na jamaa zao na wengine kujeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari matano, iliyotokea katika eneo la Igawilo Mjini Mbeya siku ya tarehe 7 Septemba, 2018 na kusababisha vifo vya watu 15 na kujeruhi wengine.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Kangi Alphaxard Lugola, (MB), kwa masikitiko makubwa anatoa pole kwa familia zote zilizopoteza wapendwa wao na kuwatakia majeruhi wote ahueni ya haraka ili warejee katika hali zao za kawaida na kuendelea na shughuli zao za kujenga nchi.

“Natoa pole nyingi kwa Watanzania wenzangu waliowapoteza wapendwa wao katika ajali hii na nawatakia majeruhi wote afya njema na wapate ahueni haraka ili waweze kurejea katika hali zao za kawaida”.

“Ni wakati muafaka kwa Watanzania wenzangu, Wasimamizi wa Sheria za Usalama Barabarani na Madereva kutokatishwa tamaa na ajali hii na badala yake changamoto hii iwafanye waongeze umakini barabarani, kuongeza umadhubuti katika usimamizi wa Sheria ya Usalama barabarani kwa kuchukua hatua kali zaidi kwa madereva wazembe na askari wasiotimiza wajibu wako wa kuhakikisha magari mabovu hayaruhusiwi kutembea barabarani”.

Mwenyezi Mungu azipe roho za ndugu zetu pumziko la amani. Amina

Imetolewa na:

Meja Jenerali Jacob G. Kingu, ndc 
KATIBU MKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...