Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
MRADI wa Kimataifa wa Uhifadhi wa Mazingira Asili wa (Interact-Bio) chini ya Baraza la Kimataifa la Mazingira utashiriki katika maonyesho ya sekta ya ujenzi yatakayofanyika kwa siku tatu jijini Dar es Salaam kuanzia kesho kwa lengo la kuonyesha njia za kiubunifu za kuwawezesha wakazi wa mijini kunufaika na viumbe na mazingira asilia.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Mazingira ya Nipe Fagio, Bi. Ana Rocha amesema leo kwenye mkutano na waandishi wa habari kwamba mradi huo umejenga bustani ya wima, gudulia la kuhifadhia mbolea na kifaa cha makazi ya wadudu (insect hotel) ili kuwawezesha wakazi wa jiji la Dar es Salaam watakotembelea maonyesho hayo kujionea namna ya kujumuisha na kunufaika na viumbe asili katika maisha ya mijini.

“Tunashirikiana na Halmashauri za Miji katika jitihada za kuongeza uelewa kuhusu manufaa yatokanayo na viumbe asili katika majiji ya Dar es salaam na Arusha pamoja na manispaa ya Moshi. Tunataka wananchi waone thamani ya kuwa na viumbe asili katika jiji na jinsi ambavyo jambo hili linaweza kutatua changamoto ya ongezeko la joto na changamoto nyingine zinazowakabili wakazi wa mijini kutokana na mabadiliko ya mazingira pamoja na hali ya hewa”. 

Amesema bustani wima ni bustani ambayo inatengenezwa kutokana na fremu za mbao, chuma, mbolea na chupa za plastiki kuotesha maua na mboga mboga kwenye kuta za nyumba au nguzo ikiwa ni njia mbadala wa kupanda mimea hiyo ardhini. Mbinu hii ya ubunifu inaweza kutumika kuweka mpaka wa mimea kati ya maeneo tofauti na kutoa nafasi kwa mimea hiyo kustawi huku ikiwasaidia wakazi wa mijini kutumia vizuri nafasi ndogo waliyonayo kwa ajili ya bustani.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mazingira wa Nipe Fagio, Bi Ana Rocha (kulia) akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya mradi wa kimataifa wa uhifadhi wa Mazingira ya Asili wa “Interact Bio”. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mazingira wa Nipe Fagio, Bi Ana Rocha (kulia) akiwaonyesha waandishi wa habari Bustani wima ambayo imetengenezwa kutokana na fremu za mbao,chuma, mbolea na chupa za plastiki, na Kifaa cha Makazi ya wadudu ikiwa ni Mradi wa kimataifa wa uhifadhi wa Mazingira ya Asili wa “ Interact Bio”. 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mazingira wa Nipe Fagio, Bi Ana Rocha (Kulia) wakionyesha bango linaloonyesha umuhimu wa uoto asili katika majiji ya Dar es Salaam, Arusha na Moshi, (Kushoto) ni Afisa Tehama wa Taasisi ya Nipe Fagio Olarip Tomito.
Moja ya bustani za wima iliyotengenezwa na inazotarajiwa kufundishwa kwa wananchi ili zichangie katika utunzaji wa mazingira. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...