Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MAMLAKA ya Udhibiti ya Usafiri wa Maji na Nchi Kavu (Sumatra) imesema kuwa inafanyia kazi agizo la Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye kuhusiana na safari za masafa ya kuanzia masaa nane kuanza kuondoka katika kituo cha mabasi Ubungo saa 11 pamoja na kuanza kwa safari za Dodoma-Dar es Salaam kwa masaa 24.

Akizungumza na Michuzi Blog kwa njia ya simu Mkurugenzi wa Udhibiti wa Usafiri wa Barabara wa Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), Johansen Kahatano amesema kuwa katika wiki mbili alizotoa Naibu Waziri huyo wanaendelea kufanyia kazi kwa kushirikiana na jeshi la polisi na baada ya hapo watawatangazia wananchi.

Amesema kuwa katika kuanza huko wanaangalia mazingira ya usalama wa abiria kutoka muda uliozoeleka na kuingia muda mwingine wa kufanya safari hizo.

“Bado tunaendelea kufanyia kazi agizo la Naibu Waziri Nditiye na tukimaliza kazi kuangalia mazingira ya usafiri huo kuanza safari saa 11 na ile ya Dodoma ya masaa 24 ni kuwatangazia wananchi ambayo itafabywa na (Sumatra)”amesema Kahatano.

Aidha amesema wananchi waendelee kuendelea na muda uliokuwepo katika kituo cha mabasi ubungo kuondoka saa 12 kukiwa na mabadiliko watapata taarifa juu ya mabadiliko hayo.
Basi zikikaguliwa kabla ya kuanza kuondoka katika kituo cha mabasi Ubungo kwa ajili ya safari za kwenda mikoa mbalimbali ya hapa nchini na nje ya nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...