Walinzi katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC) ya Jijini Mwanza wamemnasa mtu mmoja ambaye inadaiwa amekuwa akijifanya daktari na kujichumia fedha kwa kuwarubuni wagonjwa na watu wenye shida mbalimbali.
Wauguzi na Madaktari walikuwa wakimfuatilia kwa muda mrefu wakishirikiana na walinzi wa hospitalini hapo, baada ya kupokea malalamiko ya mara kwa mara toka kwa wananchi wanaokimbilia hospitalini hapo kupata huduma ndipo JUZI Jumatano ya tarehe 3/september 2018) majira ya saa moja usiku, wakamnasa daktari huyo feki akiwa katika harakati zake za kufanya kinachodhaniwa kuwa ni utapeli.
Joseph Samwel (26) alikamatwa kwenye viunga vya hospitali hiyo akiwa kwenye harakati za kujifanya mtoa huduma akiwa na sare zenye kufanana na watumishi hospitalini hapo. Lucy Mogele ni Afisa Uhusiano wa Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza naye anafunguka zaidi juu ya daktari huyu feki......
GSENGOtv
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...