Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) imedhamiria kuendelea kuimarisha huduma zake katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano hasa katika ujenzi wa Viwanda kwa kuhakikisha kuwa huduma hiyo inafika maeneo ya Viwanda na kwa wananchi kwa kiwango kinachotakiwa.

Akizungumza katika kipindi cha mizani kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Afisa  Mtendaji mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema kuwa wamejipanga kuhakikisha kuwa maeneo yote yanafikiwa na huduma ya maji safi na salama yakiwemo ya Viwanda na maeneo ya pembezoni  mwa Jiji la Dar es Salaam ambapo tayari hatua zimechukuliwa katika kutekeleza azma hiyo.

 “Tumejipanga kuhakikisha kuwa  hata wananchi wasio na uwezo  wanafikiwa na huduma ya maji kwa njia ya mkopo ambapo tunawaunganishia maji na wanalipia kidogo kidogo hivyo mwananchi hatakuwa na sababu ya kukosa maji na hii ndiyo dhamira ya Serikali yetu;” Alisisitiza  Mhandisi Luhemeja.

Aliongeza kuwa Mamlaka hiyo pia ina miradi yakupeleka maji katika maeneo rasmi ya viwanda katika mkoa wa Pwani ambapo kuna miradi katika Wilaya za Kisarawe, Kibaha,Bagamoyo na Mkuranga ili kuchochea ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...