Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa ikiwa katika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma ambapo imekutana na Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa ya Ofisi ya Rais, Bodi ya Mishahara na Maslahi katika Utumishi wa Umma.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Mwanne Nchemba akisisitiza jambo katika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma. Kamati hiyo imekutana na Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa ya Ofisi ya Rais , Bodi ya Mishahara na Maslahi katika Utumishi wa Umma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akitolea ufafanuzi hoja za wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakati Kamati hiyo ilipokutana na Wizara yake kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa ya Ofisi ya Rais , Bodi ya Mishahara na Maslahi katika Utumishi wa Umma.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...