Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (kushoto), akizungumza na Wakuu wa Idara na Taasisi pamoja na maafisa mbalimbali wa Wizara hiyo, katika kikao cha kupitia taarifa ya utekelezaji wa muundo mpya wa Wizara hiyo kilichofanyika jijini Dodoma leo. Kushoto kwa Katibu Mkuu, ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhan Kailima, akifuatiliwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye. Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Issa Ng’imba.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhan Kailima akizungumza katika kikao cha kupitia taarifa ya utekelezaji wa muundo mpya wa Wizara hiyo kilichofanyika jijini Dodoma leo. Kikao hicho kilihudhuriwa na Wakuu wa Idara na Taasisi zilizopo ndani ya Wizara hiyo. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (katikati), akizungumza na Wakuu wa Idara na Taasisi pamoja na maafisa mbalimbali wa Wizara hiyo, katika kikao cha kupitia taarifa ya utekelezaji wa muundo mpya wa Wizara hiyo kilichofanyika jijini Dodoma leo. Watatu kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhan Kailima, na watatu kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Issa Ng’imba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali, Jacob Kingu (wapili kulia), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhan Kailima (kulia), pamoja na Wakuu wa Idara na Taasisi pamoja na maafisa mbalimbali wa Wizara hiyo, wakimsikiliza Mwasilishaji wa taarifa kwa niaba ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, ASF Athuman Nassa, alipokua anawasilisha katika kikao cha kupitia taarifa ya utekelezaji wa muundo mpya wa Wizara hiyo kilichofanyika jijini Dodoma leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...