Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kulia) akielekeza jambo wakati alipokuwa akiwapatia mawaidha wachezaji wa Timu ya Mpira wa Kikapu (Basket Ball) ya Benki hiyo, inayoshiriki michuano ya mabenki (Bankers Basketball League) iliyoanza kutimua vumbi leo katika viwanja vya Gymkana, Ocean Road jijini Dar es salaam. Nsekela alifika uwanjani hapo kuwapa hamasa vijana wake na kuwatakia ushindani uliokuwa mwema katika mchezo huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akiepana mkono na mmoja wa wachezaji wa Timu ya Mpira wa Kikapu (Basket Ball) ya Benki hiyo, inayoshiriki michuano ya mabenki (Bankers Basketball League) iliyoanza kutimua vumbi leo katika viwanja vya Gymkana, Ocean Road jijini Dar es salaam.
Kikosi cha Timu ya Benki ya CRDB.
Mchezaji wa Timu ya Mpira wa Kikapu ya Benki ya CRDB, Godwin Semunyu (kushoto) akiwa katika harakati za kutoka ngome ya wapinzani wao Benki ya DTB, katika mchezo uliopigwa leo katika viwanja vya Gymkana, Ocean Road jijini Dar es salaam.







Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...