Na Khadija Seif,Globu ya jamii

TAASISI isiyo ya kiserikali SUKOS inayomilikiwa na Kamishna mstaafu wa Jeshi la Polisi Suleiman Kova imezinduliwa rasmi jijini Dar es salaam.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Kova Taasisi hiyo ilianzishwa mwaka 2014  ambayo inatoa , huduma ya uokoaji,usimamizi,uhamasishaji wa jamii kuhusiana na namna ya kukabiliana na maafa ya aina mbalimbali ikiwa ni harakati za kuunga mkono juhudi za Serikali kukabiliana na maafa na majanga .

Kova ameeleza mabadiliko ya nchi yetu kwa sasa   haiwezi kuepukana na majanga na kutokana na uzoefu na  utendaji wake wa kazi na Jeshi la Polisi lilitoa msaada wa hali na mali kuhakikisha wananchi wanarudi Kwenye maisha yao ya kila siku.

 Kova ameyataka  kwa mashirika yasiyo ya Serikali  kusaidia wananchi wanaofikwa na kadhia hiyo ili kupata hifadhi kwa muda pamoja na chakula.Hata hivyo  ametoa pole kwa  ajari iliyotokea Mkoa wa Mwanza kwa kuzama kwa kivuko cha MV. Nyerere mkoani Mwanza Katika Wilaya ya Ukerewe  na kusababisha athari kubwa ya kimaisha na mali katika jamii.

Aidha, amefafanua kazi ya taasisi hiyo ni  kutoa elimu kuhusu namna ya kujiokoa katika maafa ikishirikiana na kampuni ya CocaCola,Taasisi ya Mpango wa Taifa ya Damu salama,na Cops Security.Pia amesema tarehe sita kutakua na  mbio za mwendopole ambazo zitafanya katika Uwanja Taifa kuelekea viwanja vya Jakaya M. Kikwete saa moja asubuh pamoja na tukio la uchangiaji wa damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa hospitalini.

Kova ametoa rai kwa wananchi kujitokeza Oktoba  6 ili kujifunza vingi likiwemo suala la kujikinga na kujiokoa kwenye majanga na maafa yatakayotokea mahali popote .
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...