SHULE ya Msingi Tusiime imeendelea kufanya vizuri kitaaluma baada ya kufanikiwa kuwa ya 13 kitaifa kati ya shule 10,090 na kuwa ya pili kwa Mkoa wa Dar es Salaam ikiwa na wanafunzi wengi kuliko shule zote.
Shule hiyo pia imefanikiwa kuwa ya kwanza kwa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam kati ya shule 90 na kutoa wanafunzi bora wawili kati ya wasichana 10 bora kitaifa na mvulana mmoja kwenye 10 bora kitaifa wavulana.
Wasichana wawili wa shule hiyo waliongia 10 bora ni Hamisa Kasele aliyeshika nafasi ya nne na Kareen Gabriel aliyeshika nafasi ya tano kitaifa.
Shule hiyo imekuwa ya 13 kitaifa ikiwa na jumla ya wanafunzi 243 ambapo 239 wamepata wastani wa alama A.Shule nyingi zilizoingia 10 bora zilikuwa na wastani wa wanafunzi 70,60, 65 kwa mujibu wa matokeo hayo yaliyotangazwa na Baraza la Taifa la Mitihani NECTA hivyo Tusiime kuwa shule yenye wanafunzi wengi zaidi.
Baadhi ya wazazi waliozungumza na gazeti hili kuhusu matokeo hayo ya Tusiime walisema wamefurahishwa na matokeo ya shule hiyo ya darasa la saba mwaka huu hasa kwa wanafunzi wote 239 kupata wastani wa alama A.
Mwalimu wa Taaluma wa Shule ya Msingi Tusiime, Maxon Binomtonzi akiwapa matokeo ya darasa la saba wanafunzi wa shule hiyo ambayo ilikuwa na watahiniwa 243 imefanikiwa kuwa ya 13 kitaifa kati ya shule 10,090 nchini na kuwa ya pili Mkoa wa Dar es Salaam na ya kwanza Wilaya ya Ilala.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...