Na Estom Sanga- Simiyu

Walengwa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF waliopata fursa ya kushiriki katika maonyesho yaliyoandaliwa na Shirika la Kuhudumia viwanda vidogo vidogo –SIDO yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu wamesema maonyesho hao yamekuwa ya manufaa makubwa kwao na kuishukuru serikali kupitia TASAF kwa kuwawezesha .

Maonyesho hayo yaliyofunguliwa na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassimu Majaliwa yanawashirikiwa Wajasiliamali wadogo na wakati ambao wamepata fursa ya kuonyesha bidhaa wanazozalisha na pia kujifunza teknolojia rahisi ya kutengeneza bidhaa mbalimbali kwa lengo la kutimiza azma ya serikali ya kukuza sekta ya viwanda nchini.

Bidhaa zilizoletwa na Walengwa wa TASAF kwenye maonyesho hayo hutengenezwa kwa njia ya vikundi baada ya kuwezeshwa na Mfuko huo wa Maendeleo ya Jamii kama njia mojawapo ya kuinua kipato cha Walengwa na kupunguza adha ya umaskini. Miongoni mwa bidhaa ambazo Walengwa hao wa TASAF wanaonyesha , ni pamoja na sabuni za vipande na maji, majani ya chai yaliyozalishwa kutokana na mmea wa mchaichai,vyungu,bidhaa za ususi ,nguo aina ya batiki,urembo na mafuta ya kupakaa.

Wakizungumza kwenye banda hilo la TASAF, Walengwa hao wamesema fursa waliyoipata imewawezesha siyo tu kuuza na kupata soko la bidhaa zao, bali pia wameweza kujifunza mbinu za kuendesha shughuli za uzalishaji mali wenye tija jambo ambalo wamesema litainua kipato chao. “tunashukuru sana TASAF kwa kutufungua macho tumeweza kujua namna bora ya kuendesha shughuli zetu za kuzalisha bidhaa na kupata soko “amesema mmoja wa Walengwa ambaye kikundi chake kinajishughulisha na uzalishaji wa mafuta ya kujipakaa na sabuni.

Wakizungumzia changamoto wanayokabiliana nayo katika utekelezaji wa shughuli za uzalishaji wa bidhaa zao, Walengwa hao wametaja tatizo la uduni wa vifungashio vya bidhaa ambayo wamesema ikipatiwa ufunguzi watakuwa wamepiga hatua kubwa kuelekea katika maendeleo ya uhakika. “tazama hivi sasa tunalazimika kuweka sabuni ya maji kwenye chupa za plastiki tunazookoteza baada ya kutumika na kutupwa na watumiaji wengine jambo hilo linapunguza sana ubora wa bidhaa zetu” amelalamika mlengwa huyo wa TASAF.

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF umekuwa na utaratibu wa kuwashirikisha baadhi ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko huo kwenye maonyesho mbalimbali ya Wajasiliamali ili kuwawezesha Walengwa hao kujifunza na kuonyesha bidhaa wanazozalisha kwa lengo la kupata pia soko la bidhaa zao.

Baadhi ya Walengwa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF waliopata fursa ya kushiriki katika maonyesho yaliyoandaliwa na Shirika la Kuhudumia viwanda vidogo vidogo –SIDO yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu wamesema maonesho hayo yamekuwa ya manufaa makubwa kwao na kuishukuru serikali kupitia TASAF kwa kuwawezesha .
 Baadhi ya Walengwa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF waliopata fursa ya kushiriki katika maonyesho yaliyoandaliwa na Shirika la Kuhudumia viwanda vidogo vidogo –SIDO yanayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu,wakiwa na baadhi ya bodhaa zao walizozitengeneza,aidha wamesema maonesho hayo yamekuwa ya manufaa makubwa kwao na kuishukuru serikali kupitia TASAF kwa kuwawezesha .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...