Uongozi wa Chuo cha Kimataifa cha Sayansi na Biashara cha Nchini Oman umekusudia kuanzisha chuo chengine kipya cha Kimataifa Visiwani Zanzibar kitachopewa jina la American and Europe of  East Africa kwa lengo la kutanua Sekta ya Elimu ndani ya Ukanda wa Afrika Mashariki.

Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Biashara cha Nchini humo Dr. Muneer Moh’d Al – Naamany alitoa kauli hiyo wakati Ujumbe aliouongoza wa Chuo hicho ulipofanya mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar.

Dr. Muneer Moh’d Al – Mastar alisema Zanzibar lazima iwe kituo cha Elimu katika Ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Bara la Afrika kitakachomjengea uwezo wa ajira ya kuaminika mahali popote Duniani Mwanafunzi aatakayemaliza masomo yake kwenye Chuo hicho.

Alisema mazingira ya kumfinyanga Mwanafunzi katika muelekeo wa chuo hicho kinachokusudiwa kuanzishwa Zanzibar unatokana na uzoefu wa miaka 20 tokea kuanzishwa kwa Chuo chao chenye Wahadhiri kutoka pembe zote za Dunia wanaofundisha kwenye Taasisi yao.

Mkuu huyo wa Chuo cha Sayansi na Biashara cha Oman mwenye Asili ya Zanzibar alimueleza Balozi Seif kwamba Uongozi wa Chuo chake umefikiria Mpango huo kwa nia ya kuirejeshea hadhi yake Zanzibar kuwa Kituo cha masuala mengi katika enzi zilizopita hasa harakati za Biashara na usafiri uliokuwa ukiunganisha Dunia.

Naye kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Biashara cha Nchini Oman Dr. Ahmed Al – Naamany alisema mfumo wa ufundishaji utakaotumika utampa uwezo Mwanafunzi kuendelea na masomo yake hata akiwa nje ya Zanzibar.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Kulia akizungumza na Uongozi wa Chuo cha Kimataifa cha Sayansi na Biashara  cha Nchini Oman uliofika Ofisini kwake Vuga kwa mazungumzo ya kuataka kuanzisha Chuo Kikuu Visiwani Zanzibar.
 Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Biashara cha Nchini humo Dr. Muneer Moh’d Al – Naamany wa Pili kutoka Kulia akielezea msimamo wa Uongozi wa Chuo chake kutaka kuanzisha Chuo Kikuu Visiwani Zanzibar.
 Dr. Muneer Moh’d Al – Naamany akisisitiza jambo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar.
 Naibu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Biashara cha Nchini Oman Dr. Ahmed Al – Naamany akimueleza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mh. Riziki Pembe Juma aliyeshiriki mazungumzo hayo fursa zitakazopatikana katika mafunzo yatakayotolewa na Chuo hicho.
  Dkt. Muneer Moh’d Al – Naamany akifafanua zaidi malengo ya Chuo chake mbele ya  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...