Mkuu
wa Wilaya ya Pangani Mh. Zainab Abdalah ametembelea uongozi wa Benki ya
Maendeleo ya kilimo nchini kufanya kikao kilichomkutanisha Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Ndg. Japhet Justine na viongozi
waandamizi ambao kwa pamoja wameahidi kuifanya Pangani wilaya ya mfano
na ya kimkakati kwenye mipango yao.
..
Kikao
hiki kimetoka na maazimio mazito kuelekea mapinduzi ya kilimo Pangani
na moja kwa moja Mkurugenzi amekubali kua tayari kujenga kituo kikubwa
cha ukusanyaji maziwa Pangani eneo la Madanga.Aidha kikao kimeadhimia kuisaidia sekta ya uvuvi Pangani kuhakikisha inaleta mapinduzi ya uchumi kwa wavuvi.
..
Muhimu
zaidi mazungumzo yamefanyika na kuweka misingi itakayowasaidia vijana
wa Pangani hasa waliotayari kuungana na kunufaika na mipango ilioazimiwa
na uongozi mzima kuahidi hivi karibuni kufika Pangani kuchagiza
yaliopangwa na kujionea nini zaidi wanaweza kufanya na Pangani.
..
Mkuu
wa Wilaya Pangani amemshukuru Kaimu Mkurugenzi Mtendaji kwa ufanisi
wake na utayari aliounesha,kasi uwajibikaji na zaidi alivo tayari
kujitoa kwa ajili ya Maendeleo ya nchi yetu.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Ndg. Japhet Justine akiungumza na viongozi wa wilaya ya Pangani wakati wa kikao chao cha pamoja kuhusiana ushirikiano
Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah akizungumza katika kikao hicho kulia ni Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George
Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George kulia akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Ndg. Japhet Justine kushoto akiangana na Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...