Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( TAMISEMI) Mwita Wairata amewasisitiza wafanyabiashara na wenye Viwanda nchini kulipa kodi ya maendeleo ili Serikali iwe na uwezo wa kufanya miradi ya kimaendeleo ambayo itasaidia wananchi wengi.

Waitara ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa kuelekea katika kilele cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo(TCCIA) ambapo amesema ili Serikali iongeze ufanisi katika kuhudumia jamii wafanyabiashara na wawekezaji katika maenneo mbalimbali wanapaswa kulipa kodi ya mapato ambayo pamoja na kusaidia uongezwaji wa miradi ya maendeleo pia itaboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Amesema chama hicho kimekuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha uchumi wa Taifa na kuunga mkono juhudi za Seikali ya Awamu ya tano ya Rais Dk.John Magufuli inayosisitiza uchumi wa Viwanda.“Wafanyabiashara lipeni kodi ya maendeleo, Kodi ndio itatufanya kuwawekea mazingira mazuri ya uwezeshaji na hatimaye mfanye biashara zenu kwa ufanisi mkubwa, sisi tutaendelea kuwawezesha kwani chama chenu ni muhimu sana katika kukuza ustawi wa kijamii,"amesema Waitara.

Naibu Waziri TAMISEMI Mwita Waitara (wa pili kushoto) akisalimiana na  Mkuu wa Kitengo cha Biashara benki ya KCB Masika Mkulu.Wa kwanza kushoto ni Kaimu Rais wa Chama cha Wafanyabiashara wenye viwanda na kilimo Octavian Mshiu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...