*Lengo ni kukumbusha na kusisitiza umuhimu wa wadau kuzingatia sheria za usalama barabarani, wanafunzi watoa neno

KLABU ya Usalama barabarani ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge wametoa elimu ya usalama wa barabarani kwa madereva wa magari na bodaboda kuzingatia sheria za usalama barabarani haswa vivuko vya watembea kwa miguu ili kuepusha ajali na vifo.

Pia wametoa elimu hiyo wanafunzi hao wametoa zawadi ya madaftari,kalenda na mabegi ya shule yenye jumbe mbalimbali zinahusu masuala ya usalama barabarani kwa madereva mbalimbali kama sehemu ya kuhakikisha elimu ya usalama barabarani inafika kila mahali.

Wanafunzi hao 18 ambao ni mabalozi wa usalama barabarani kutoka kwenye Klabu hiyo wametoa elimu hiyo na zawadi hizo Novemba 10, 2018 wakiwa kwenye Kituo cha Mafuta cha Puma kilichopo Upanga jijini Dar es Salaam ambapo madereva waliofika kuweka mafuta walikuwa wakipewa elimu hiyo inayohusu usalama barabarani.

Akizungumza wakati wa utoaji elimu kwa madereva, Rosenice Senyandumi ambaye ni Mwanafunzi wa shule hiyo amesema ajali za barabarani zimekuwa zikikatisha uhai wa binadamu wasio na hatia wakiwemo wanafunzi na mara nyingi huchangiwa na madereva wazembe.

"Ajali za barabarani zinapunguza nguvu kazi ya Taifa na kuathiri watoto kwa kuwa wengi hupoteza wategemezi wao na wakati mwingine watoto wenyewe kupoteza maisha au kupata ulemavu wa kudumu kutokana na ajali," amesema.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Energy Tanzania, Dominic Dhanah akishuhudia wakati wanafunzi kutoka Klabu ya Usalama barabarani ya Shule ya Msingi Bunge Raymond Chuwa kulia na Abbas Abdalla wa darasa la tano wakitoa elimu ya usalama barabarani na kugawa zawadi za madaftari na mabegi kwa dereva Mary Carneiro aliyefika kwenye kituo cha mafuta cha Puma Upanga jijini Dar es salaam ili kujipatia huduma ya mafuta aliyesimama nyuma katikati ni Boniface Mench Meneja Usalama Kazini Puma.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania, Dominic Dhanah akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari mara baada ya kushuhudia wanafunzi hao wakati wakitoa elimu ya Usalama barabarani kwa madereva.

Mwanafunzi Samira Jaffari akitoa elimu ya usalama barabarani na kugawa zawadi ya madaftari kwa mmoja wa Madereva waliofika kwenye kituo cha mafuta cha Puma Upanga ili kujipatia huduma ya mafuta.
Loveness Hoyange Meneja Rasilimali Watu Kampuni ya Puma Energy Afrika Mashariki na Boniface Mench Meneja Usalama Kazini Puma wakikabidhi zawadi mbalimbali za Mabegi, Madaftari na Kalenda kwa wanafunzi wa Kalabu ya Usalama Barabarani kutoka shule ya msingi Bunge ili kugawa kwa madereva wakati walipokuwa wakitoa elimu ya usalama barabarani katika kituo cha mafuta cha Puma Energy Upanga jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...