Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Wataalamu mbalimbali wa Afya wakiwemo Madaktari bingwa wa Moyo kutoka nchini Israeli, pamoja na Madaktari wawili kutoka nchini Marekani, Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuzungumza nao na kuwashukuru kwa huduma wanayoitoa nchini. Wengine katika picha ni Balozi wa Israel hapa nchini Noah Gal Gendler wanane kutoka (kushoto) waliosimama mstari wa mbele Naibu Waziri wa Wizara ya Afya Dkt. Faustine Ndungulile watisa kutoka kulia mstari wa mbele.
.
Madaktari hao kutoka Taasisi ya Save a Child’s Heart ya Israel pamoja na Madaktari kutoka Marekani wakiwa Ikulu jijini Dar es Salaam kabla ya kuanza mazungumzo yao na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa zawadi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa Mohamed Janabi mara baada ya mazungumzo ujumbe wa Madakatari kutoka Taasisi ya Save a Child’s Heart ya Israel pamoja na Madaktari kutoka Marekani Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa Barua ya Shukrani Balozi wa Israel hapa nchini Noah Gal Gendler ili aiwasilishe kwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwa ajili ya kushukuru kutokana na mchango wa Taasisi hio ya Save a Child’s Heart.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...