Na James Ndege - Shinyanga
TFDA inaendesha mafunzo ya siku mbili kwa wajasiriamali wadogo wa usindikaji wa vyakula mkoani Shinyanga ikiwa ni mojawapo ya mikakati yake ya kuwezesha ukuaji wa Sekta ya  viwanda nchini kwa wasindikaji 100 wa mkoa huo  kuanzia tarehe 22 – 23 Novemba 2018 katika Ukumbi wa SIDO Mkoa, Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Mafunzo hayo yalifunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Bi. Jasinta Mboneko kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Zainab R. Telack ambaye aliwaasa wasindikaji wa vyakula hao kutumia fursa hiyo kwa ukamilifu ili waweze kukidhi vigezo muhimu vya kisheria na kuzalisha bidhaa bora, salama na zenye ufanisi ili kukidhi soko la ndani na nje ya nchi jambo litakalochangia ukuaji wa uchumi wa nchi lakini pia kulinda afya ya jamii kwa kuwa TFDA ipo karibu na kundi hili muhimu katika uanzishaji wa viwanda nchini kwa kutatua changamoto zao.
“Kafanyeni kazi zenu kwa kufuata mafundisho mtakayopewa, tunawategemea kwamba ninyi mtakuwa mabalozi wazuri kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wengine, kwenye Mkoa wetu tumejipanga kuhakikisha kwamba kila mmoja anafanya shughuli zake zilizo halali, hakuna ujanja ujanja kwenye Serikali ya awamu hii ya Awamu ya  Tano inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Nadhani ninyi nyote mmeona kwenye vyombo vya habari kilichotokea Kahama kwa Wafanyabishara wasiotaka kufuata sheria.
Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Jasinta Mboneko akifungua mafunzo ya siku mbili tarehe 22 – 23/11/2018 kwa Wajasiriamali Wadogo wa Usindikaji wa Vyakula mkoani Shinyanga, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Zainab R. Telack katika Ukumbi wa SIDO wa Mkoa wa Shinyanga. Kulia, ni Mkaguzi Mkuu wa Chakula wa TFDA, Lazaro Mwambole na kushoto ni Mwenyekiti wa mafunzo hayo Juma Nyankanga
Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula Justin Makisi akisisitiza jambo kwa washiriki wa mafunzo (hawapo pichani). Kushoto, ni Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Bi. Jasinta Mboneko na kulia ni Meneja wa TFDA Kanda ya Ziwa, Moses Mbambe
Sehemu ya wasindikaji wa vyakula wa mkoa wa Shinyanga wakifuatilia mada zilizotolewa na TFDA katika mafunzo hayo.
Sehemu ya picha ya pamoja baina ya Mgeni Rasmi, Watumishi wa Serikali na Wasindikaji wa chakula wa mkoa wa Shinyanga.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...