Na Agness Francis, Glogu ya jamii

UONGOZI wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF ) umemtangaza kuchaguliwa kwa mwamuzi Jonesia Rukyaa kuchezesha Fainali za Afrika za Wanawake zitakazofanyika nchini Ghana.

Rukya ambaye ni muauzi kutoka mkoani Kagera ambaye amekuwa akiminiwa sana katika umakini wa kazi yake na hasa katika kuchezesha mechi za Ligi kuu Tanzania bara.

Kwa mujibu wa TFF mwamuzi huyo amechaguliwa katika orodha ya Waamuzi wa katikati kuchezesha michezo ya fainali za Afrika za wanawake zitakofanyika nchini Ghana. Ambapo jumla ya Waamuzi 13 waliochaguliwa ni wa kati Kati na wasaidizi ni 12.

Hivyo TFF imesema fainali hizo pia zitatumika kupata timu zitakazowakilisha Afrika kwenye Fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake zitakazofanyika mwakani nchini Ufaransa.

Ambapo Washindi watatu wa juu ndio watakaofuzu kushiriki Kombe la Dunia..

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...