Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

BINTI Filamu Foundation imeandaa tamasha maalum liitwalo 'Kataa Mihadarati Festival' litakalofanyika Desemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania kuhsu athari za dawa za kulevya.

Katika kuhakikisha tamasha hilo linafanikiwa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini limetangaza kuungana na Binti Filamu kufanikisha lengo hilo na huku likifafanua jukumu la kupiga vita biashara ya matumizi ya dawa hizo ni la kila mmoja wetu.

Akizungumzia tamasha hilo leo jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea amesema wanatarajia kuwepo kwa makundi ya watu mbalimbali siku hiyo wakiwamo wasanii maarufu.

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi na Vijana Anthony Mavunde.Pia Naibu Waziri katika ofisi hiyo anayeshughulikia walemavu Stella Ikupua atahudhuria tamasha hilo.

"Tamasha litaanza saa tatu kamili asubuhi ya Desemba 28 mwaka huu wa 2018, wasanii mbalimbali wa Bongo Movie na Bongo Fleva watakuwepo ili kufanikisha tamasha hilo.Pia waliokuwa wanatumia dawa hizo na sasa wameacha watatoa ushahidi wa athari za dawa za kulevya,"amesema Thea.

Thea amesema Binti Filamu inayo dhamana ya kuhakikisha inashiriki kutoa elimu kuhusu athari za dawa za kulevya huku akifafanua kuwa wapo baadhi ya wasanii wamekuwa wakihusishwa na matumizi ya dawa za kulevya.
Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea akieleze malengo ya kuandaa tamasha hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo kushoto ni Rais wa Shirikisho la Filamu nchini Tanzania TAF Bw Simon Mwakifwamba na katikati niKamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi

Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu tamasha maalum liitwalo ‘Kataa Mihadarati Festival’ litakalofanyika Desemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania kuhsu athari za dawa za kulevya katikati ni Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini Tanzania TAF Bw Simon Mwakifwamba akizungumza machache katika mkutano huo katikati ni Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi na kulia ni Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bi Joyce Fisoo akifafanua jambo kuhus tamasha hilo la kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya katika mkutamo huo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...