Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
BINTI Filamu Foundation imeandaa tamasha maalum liitwalo 'Kataa Mihadarati Festival' litakalofanyika Desemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania kuhsu athari za dawa za kulevya.
Katika kuhakikisha tamasha hilo linafanikiwa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini limetangaza kuungana na Binti Filamu kufanikisha lengo hilo na huku likifafanua jukumu la kupiga vita biashara ya matumizi ya dawa hizo ni la kila mmoja wetu.
Akizungumzia tamasha hilo leo jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea amesema wanatarajia kuwepo kwa makundi ya watu mbalimbali siku hiyo wakiwamo wasanii maarufu.
BINTI Filamu Foundation imeandaa tamasha maalum liitwalo 'Kataa Mihadarati Festival' litakalofanyika Desemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania kuhsu athari za dawa za kulevya.
Katika kuhakikisha tamasha hilo linafanikiwa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini limetangaza kuungana na Binti Filamu kufanikisha lengo hilo na huku likifafanua jukumu la kupiga vita biashara ya matumizi ya dawa hizo ni la kila mmoja wetu.
Akizungumzia tamasha hilo leo jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea amesema wanatarajia kuwepo kwa makundi ya watu mbalimbali siku hiyo wakiwamo wasanii maarufu.
Mgeni
rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu
anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi na Vijana Anthony Mavunde.Pia Naibu
Waziri katika ofisi hiyo anayeshughulikia walemavu Stella Ikupua
atahudhuria tamasha hilo.
"Tamasha litaanza saa tatu kamili asubuhi ya Desemba 28 mwaka huu wa 2018, wasanii mbalimbali wa Bongo Movie na Bongo Fleva watakuwepo ili kufanikisha tamasha hilo.Pia waliokuwa wanatumia dawa hizo na sasa wameacha watatoa ushahidi wa athari za dawa za kulevya,"amesema Thea.
"Tamasha litaanza saa tatu kamili asubuhi ya Desemba 28 mwaka huu wa 2018, wasanii mbalimbali wa Bongo Movie na Bongo Fleva watakuwepo ili kufanikisha tamasha hilo.Pia waliokuwa wanatumia dawa hizo na sasa wameacha watatoa ushahidi wa athari za dawa za kulevya,"amesema Thea.
Thea amesema Binti Filamu inayo
dhamana ya kuhakikisha inashiriki kutoa elimu kuhusu athari za dawa za
kulevya huku akifafanua kuwa wapo baadhi ya wasanii wamekuwa
wakihusishwa na matumizi ya dawa za kulevya.
Mkurugenzi
wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea akieleze malengo
ya kuandaa tamasha hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo
kushoto ni Rais wa Shirikisho la Filamu nchini Tanzania TAF Bw Simon
Mwakifwamba na katikati niKamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi
Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu tamasha maalum liitwalo ‘Kataa Mihadarati Festival’ litakalofanyika Desemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania kuhsu athari za dawa za kulevya katikati ni Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini Tanzania TAF Bw Simon Mwakifwamba akizungumza machache katika mkutano huo katikati ni Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi na kulia ni Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bi Joyce Fisoo akifafanua jambo kuhus tamasha hilo la kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya katika mkutamo huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...