Karibu Tuelimishane Mambo Muhimu Kadhaa Ya Kuzingatia Kabla Ya Kuanza Ujenzi

Unaweza Ku-Share Na Watu Zaidi Ujumbe Huu, Unaweza Ukawasaidia Sasa Au Hata Wakati Mwingine Kwa Namna Moja Au Nyingine


NOTE: Kufuata taratibu za kitaalamu katika UJENZI kunaweza kukusaidia kupunguza gharama za ujenzi mpaka 15% pamoja na kukuepushia hasara inayoweza kutokea mbeleni, sambamba na kukupatia kitu bora, kizuri na chenye thamani

1. Baada Ya Kuwa Umetayarisha Kiwanja Chako Kizuri Katika Eneo Ulilochagua, Anza Kujiridhisha Na Unachotaka Kujenga, kwa mfano

(i) Matumizi, jengo lako ni kwa ajili ya matumizi gani, makazi, biashara, ofisi, taasisi, starehe, godown/kiwanda n.k.

(ii) Jengo la aina gani, ghorofa au nyumba ya chini ya kawaida?

(iii) Unahitaji kuwe na vyumba vya matumizi gani(functional requirements) kama vile vyumba vingapi vya kulala pamoja na nini cha ziada kama vile movie theatre, maktaba n.k, kwa jengo la nyumba ya kuishi, au kama ni matumizi mengine ujue mahitaji yake

2. Tafuta mtaalamu wa majengo, msanifu au mbunifu majengo(architect), huyu ana utaalamu juu ya jengo, kazi zake na mipangilio yake yote ya kitaalamu. Atakushauri na kukuongezea uelewa wa sayansi ya majengo kwa ujumla

-Baada ya kumpeleka kuona eneo lako(site visit) mkajadiliana mkaelewana mwambie akafanye michoro ya mwanzo arudi mjadiliane na kujiridhisha kama kilichofanyika kimeendana na mahitaji yako, kisha mkishapitisha akafanye michoro ya 3D's(picha) za muonekano wa jengo husika uzione na ujiridhishe kama umeridhika na muonekano huo kisha ndio umruhusu amalizie michoro ya mwisho kwa ajili ya kufuatilia kibali cha ujenzi halmashauri husika
 
NB; Ni muhimu sana kujiridhisha na jengo lako usije kujuta baadaye au kujikuta unabomoa na kubadilisha baada ya kuona makosa, kwa sababu unakwenda kuweka pesa zako nyingi sana usije ukaingia gharama zaidi baadaye ambazo ungeweza kuziepuka mapema kwa kujiridhisha wakati wa michoro
Likifanyika vile unavyotaka utalifurahia na hutaona umepoteza

3. Kama jengo lako ni la ghorofa hutaishia hapo, unalazimika kumtafuta mtaalamu mwingine wa kutengeneza muundo wa mihimili ya jengo(structural engineer au mhandisi mihimili). Huyu hataongeza au kupunguza chochote ila atatumia michoro iliyofanywa na architect kutengeneza michoro ya muundo wa mihimili inayoshikilia jengo, kisha atakukabidhi michoro hiyo iliyopigwa mhuri kabisa kwa ajili ya kufuatilia kibali cha ujenzi halmashauri

4. Umeshakabidhiwa michoro yote ya msanifu/mbunifu majengo(architect) ambayo ni (architectural drawings) na ya mhandisi mihimili(structural engineer) ambayo ni (structural engineering drawings) yote ikiwa imepigwa mhuri utaenda nayo katika halmashauri yako kuomba kibali cha ujenzi ukiwa pamoja na hati yako ya kiwanja

5. Baada ya kupata kibali cha ujenzi halmashauri unaweza kuanza ujenzi lakini kama jengo lako ni la ghorofa utatakiwa kufuatilia vibali vingine kutoka kwenye bodi mbalimbali za ujenzi kutegemeana na ukubwa na matumizi ya jengo lako.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...