Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe.Omary Mgumba, Amefanya Kikao na watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mapema leo Jijini Dar es Salaam akiwa safarini kikazi kuelekea Mkoani Ruvuma.
 
Naibu Waziri Mgumba amewasitiza watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano na ueledi ili kutimiza dhima ya Serikali ya awamu ya Tano ili kuleta maendeleo katika uzalishaji wa chakula kupitia kilimo cha Uhakika cha Umwagiliaji kuelekea Tanzania ya viwanda.
 Picha ya Pamoja Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Mhe. Omary Mgumba akiwa na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Tume ya Taifa ya Umwagiaji katika Ofisi za Wizara ya Kilimo Jijini dar es Salaam.
Katika Picha Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Mhe. Omary Mgumba akiongea na watumishi wa Tume ya Taifa ya umwagiliaji (hawapo pichani) katika Ofisi za Wizara hiyo Jijiini Dar es Salaam, kushoto ni Bi Aida Tesha Afisa Utawala Mkuu wa Tume hiyo.
 Katika Picha ni baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba.
 Baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakimsikiliza Naibu Waziri wa Kilimo Mhe . Omary Mgumba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...