WADAU mbalimbali katika sekta ya elimu wanaokutana mjini Morogoro, wametakiwa kujadiliana kwa kina kuhusu mimba za utotoni, UKIMWI na Ukatili wa Kijinsia kwa kuangalia taratibu zilizopo sasa za kukabiliana na hali hiyo ili kufanya maeneo ya elimu kuwa salama na chanzo cha mabadiliko ya kitabia.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kinga wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Neema Rusibamayira katika hotuba iliyosomwa na Afisa wa Elimu Afya Mashuleni wa Wizara hiyo, Bw. Avit Maro wakati akifungua mkutano wa wadau wanaojadili kanuni, taratibu sera za taifa kuhusu mimba za utotoni, UKIMWI na ukatili wa kijinsia maeneo ya shule na vyuo.
Mkutano huo ambao umeelezwa kuwa wa kuongeza kasi kwa sekta za elimu kukabiliana na mimba za utotoni, UKIMWI na ukatili wa kijinsia katika maeneo ya shule na vyuo ni wa kamati ya uratibu ya kitaifa na uthamini wa masuala hayo na unafanyika mkoa wa Morogoro katika hoteli ya Kingsway.
Msingi wa mkutano huo ni kutafuta mkakati wa pamoja wa kuweza kuhuisha sera hizo kulingana na hali ilivyo kwa sasa ili kuweza kukabili changamoto zilizopo.
Afisa
wa Elimu Afya Mashuleni wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto, Bw. Avit Maro akitoa hotuba ya kufungua mkutano wa
wadau wanaojadili kanuni, taratibu sera za taifa kuhusu mimba za
utotoni, UKIMWI na ukatili wa kijinsia maeneo ya shule na vyuo
uliofanyika Hoteli ya Kingsway mjini Morogoro.
Mkuu
wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi
na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos akizungumza wakati
wa mkutano wa wadau wanaojadili kanuni, taratibu sera za taifa kuhusu
mimba za utotoni, UKIMWI na ukatili wa kijinsia maeneo ya shule na vyuo
uliofanyika Hoteli ya Kingsway mjini Morogoro. Kulia ni Afisa wa Elimu
Afya Mashuleni kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
na Watoto, Bw. Avit Maro, Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Unesco,
Dr. Hamisi Malebo (wa pili kulia) pamoja na Ofisa Utawala wa Elimu wa
TAMISEMI, Jeanimina Mtitu (kushoto).
Ofisa
Utawala wa Elimu wa TAMISEMI, Jeanimina Mtitu akitoa salamu kwa niaba
ya TAMISEMI wakati wa mkutano wa wadau wanaojadili kanuni, taratibu sera
za taifa kuhusu mimba za utotoni, UKIMWI na ukatili wa kijinsia maeneo
ya shule na vyuo uliofanyika Hoteli ya Kingsway mjini Morogoro.
Afisa
Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI wa Shirika la Umoja wa Mataifa la
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Herman Mathias akizungumza
jambo na washiriki wa mkutano wa wadau wanaojadili kanuni, taratibu sera
za taifa kuhusu mimba za utotoni, UKIMWI na ukatili wa kijinsia maeneo
ya shule na vyuo uliofanyika Hoteli ya Kingsway mjini Morogoro.
Program
Meneja wa kitaifa wa elimu ya afya shuleni wa Wizara ya Elimu Sayansi
na Teknolojia, Bw. Clement Mung’alo akisherehesha mkutano wa wadau
wanaojadili kanuni, taratibu sera za taifa kuhusu mimba za utotoni,
UKIMWI na ukatili wa kijinsia maeneo ya shule na vyuo uliofanyika Hoteli
ya Kingsway mjini Morogoro.
Washiriki
wa mkutano wanaojadili kanuni, taratibu sera za taifa kuhusu mimba za
utotoni, UKIMWI na ukatili wa kijinsia maeneo ya shule na vyuo
uliofanyika Hoteli ya Kingsway mjini Morogoro wakiwa katika picha ya
pamoja.KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...