Na, Khadija Seif, Globu ya jamii
MTANDAO wa Mashirika ya kupambana na matumizi mabaya ya pombe nchini (TAAnet) imetoa wito kwa Serikali kutunga sera juu ya kudhibiti matumizi mabaya ya pombe katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi zao Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika ya kupambana na Matumizi mabaya ya pombe (TAAnet) Sophia Komba amepongeza serikali kwa uamuzi waliochukua kutokana na kuzuia na kupiga maarufu juu ya uuzwaji na utumiaji wa pombe aina ya kiroba ambayo ilikua ikiua nguvu kazi ya vijana wengi Kwenye jamii kutokana na kuathirika kiakili na kimwili na kufanya vijana kuwa tegemezi na kutojihusisha na kujenga Taifa hasa kiuchumi.
Komba ameeleza kuwa matumizi mabaya ya pombe inajumuisha pombe za aina zote za kisasa pamoja na za kienyeji ambazo zina madhara kwa jamii kutokana na kusababisha ajali barabarani, familia kutengana, kusababisha magonjwa kama shinikizo la damu , kisukari, na madhara mengine ya kiafya.
Amesema kuwa "Pombe ya kienyeji inaathiri afya ya watumiaji na watengenezaji kutokana na maandalizi ya kilevi hicho kuwekwa viungo ambayo ni hatarisha kiafya na kupelekea afya zao kuwadhaifu " amesema Komba .Kwa upande wa Mwenyekiti wa chama cha Afya jamii (TPHA) Dk. Mashombo Mkamba amesema jamii inaathirika sana kutokana na matumizi mabaya ya pombe na Kwa sasa hata baadhi ya wajawazito wanajihusisha na unywaji wa pombe tatizo linalopelekea hata kizazi kitakachozaliwa kuathirika sehemu za ubongo .
Mwenyekiti wa Mtandao wa kudhibiti matumizi mabaya ya pombe (TAAnet, Sophia Komba akizungumza na waandishi wa habari kuhusu athari zitokanazo na matumizi ya pombe uliofanyika katika ofini kwao leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Afya ya jamii (TPHA) Dk.Mashombo Makamba akizungumza na waandishi wahabari kuhusu magonjwa yanayoshamiri kwa sasa na matumizi ya pombe kuwa kisababisho kikubwa.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
MTANDAO wa Mashirika ya kupambana na matumizi mabaya ya pombe nchini (TAAnet) imetoa wito kwa Serikali kutunga sera juu ya kudhibiti matumizi mabaya ya pombe katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi zao Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika ya kupambana na Matumizi mabaya ya pombe (TAAnet) Sophia Komba amepongeza serikali kwa uamuzi waliochukua kutokana na kuzuia na kupiga maarufu juu ya uuzwaji na utumiaji wa pombe aina ya kiroba ambayo ilikua ikiua nguvu kazi ya vijana wengi Kwenye jamii kutokana na kuathirika kiakili na kimwili na kufanya vijana kuwa tegemezi na kutojihusisha na kujenga Taifa hasa kiuchumi.
Komba ameeleza kuwa matumizi mabaya ya pombe inajumuisha pombe za aina zote za kisasa pamoja na za kienyeji ambazo zina madhara kwa jamii kutokana na kusababisha ajali barabarani, familia kutengana, kusababisha magonjwa kama shinikizo la damu , kisukari, na madhara mengine ya kiafya.
Amesema kuwa "Pombe ya kienyeji inaathiri afya ya watumiaji na watengenezaji kutokana na maandalizi ya kilevi hicho kuwekwa viungo ambayo ni hatarisha kiafya na kupelekea afya zao kuwadhaifu " amesema Komba .Kwa upande wa Mwenyekiti wa chama cha Afya jamii (TPHA) Dk. Mashombo Mkamba amesema jamii inaathirika sana kutokana na matumizi mabaya ya pombe na Kwa sasa hata baadhi ya wajawazito wanajihusisha na unywaji wa pombe tatizo linalopelekea hata kizazi kitakachozaliwa kuathirika sehemu za ubongo .
Mwenyekiti wa Mtandao wa kudhibiti matumizi mabaya ya pombe (TAAnet, Sophia Komba akizungumza na waandishi wa habari kuhusu athari zitokanazo na matumizi ya pombe uliofanyika katika ofini kwao leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Afya ya jamii (TPHA) Dk.Mashombo Makamba akizungumza na waandishi wahabari kuhusu magonjwa yanayoshamiri kwa sasa na matumizi ya pombe kuwa kisababisho kikubwa.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...