Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Waziri wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) Leo
tarehe 21 Disemba 2018 ametembelea studio za Kidigitali za Kumbukumbu ya
Mwalimu Nyerere na Ukombozi wa Afrika iliyozinduliwa miezi mitano iliyopita na Shirika
la Utangazaji Nchini (TBC) katika majengo yake yaliyopo barabara ya Nyerere
jijini Dar es salaam.
Mhe Hasunga ametembelea Studio hiyo yenye
kuhifadhi historia ya kumbukumbu ya ukombozi barani Afrika zilizopo katika
kanda za sauti na video ikiwa imetengenezwa kwa ushirikiano kati ya TBC na
Umoja wa Ulaya (EU), Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(UNESCO) na wadau wengine wa maendeleo.
Mkurugenzi wa huduma za Redio-TBC Bi Aisha
Dachi, amemueleza Waziri wa kilimo kuwa Kuwapo kwa studio hiyo kumelenga
kuongeza uwajibikaji, uwezo wa kupata taarifa za zamani na kuongeza uratibu wa menejimenti
ya hifadhi ya mambo muhimu ambayo ni ya urithi wa Tanzania.
Waziri
wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akitazama ubadilishaji wa hotuba za
Mwalimu Nyerere kutoka kwenye Analogi kwenda Digitali wakati
alipotembelea studio za Kidigitali za Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na
Ukombozi wa Afrika zilizopo katika ofisi za Shirika la Utangazaji Nchini
(TBC) katika majengo yake yaliyopo barabara ya Nyerere jijini Dar es
salaam, Tarehe 21 Disemba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya
Kilimo)
Mkurugenzi wa huduma za Redio-TBC Bi Aisha Dachi akimuonyesha Waziri
wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) mitambo ya makumbusho iliyopo kwenye
studio za Kidigitali za Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na Ukombozi wa
Afrika zilizopo katika ofisi za Shirika la Utangazaji Nchini (TBC)
katika majengo yake yaliyopo barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam, Tarehe 21 Disemba 2018.
Mkurugenzi
wa huduma za Redio-TBC Bi Aisha Dachi akimuonyesha Waziri wa kilimo Mhe
Japhet Hasunga (Mb) meza iliyotumiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere kwa ajili ya mahojiano iliyopo kwenye studio za
Kidigitali za Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na Ukombozi wa Afrika
zilizopo katika ofisi za Shirika la Utangazaji Nchini (TBC) katika
majengo yake yaliyopo barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam, Tarehe
21 Disemba 2018.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...