VICTOR MASANGU, KISARAWE

WAZIRI wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo amewaagiza wakurugenzi wote wa halmashauri nchini pamoja na maafisa elimu kuachana kabisa na vitendo vya kuwanyima fursa walimu ambao wanahitaji kujifunza somo la tehema na badala yake wahakikishe wanatoa vibali bila ya kuwa na ukilitimba wowote kwa lengo la kukuza teknolojia na mawasiliano.

Jafo ametoa kauli hiyo wakati wa halfa ya kukabidhi kompyuta 25 ambazo zimetolewa na serikali kupitia mfuko wa mawasilino kwa wote ambapo zitazinufaisha shule za sekondari 14 zilizopo katika halmashauri ya Kisarawe.

Jafo alibainisha kwamba lengo kubwa la serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inawajengea uwezo walimu ambapo hadi sasa tayari walimu wapatao 570 wameshapatiwa mafunzo maalumu kwa ajili ya somo la tehema ili kuendana na kasi na mabadiliko ya kiteknolojia.

“Kitu kikubwa sisi kama serikali kwa sasa tumejipanga kuhakikisha kwamba somo hili la Tehama kwa walimu linapewa kipaumbele zaidi, lakini sipendi kuona walimu wananyimwa vibali kwa ajili ya kwenda kuongeza ujuzi katika somo hilo hivyo kuanzia sasa ofisi yangu italisimamia hili na kwamba wakurugenzi wote na maafisa elimu msiwanyime vibali kabisa wapeni acheni roho mbaya,”alisema Jafo.



Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za miko na serikali za mitaa (TAMISEMI) kati kati akimkabidhi kompyuta mmoja wa walimu wa shule za sekondari,kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo katika halfa iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za miko na serikali za mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo kati kati akiwa ameshika moja ya kompyuta ambazo zmezitoa kwa niaba ya serikali, kushoto kwake ni Naibu waziri wa uchukuzi na Mawasialiano Injinia Atashasta Nditiye, na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Kisarawe Mussa Gama wa kwanza kulia akishuhudia ugawaji wa kompyuta hizo ambazo zimetolewa na serikali kupitia mfuko wa mawasiliano kwa wote ambapo shule 14 za sekondari zimeweza kunufaika na msaada huo.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...