Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii .

Kampuni ya Yapi Merkezi inayojenga Reli ya Kisasa imefanya usafi katika ufukwe wa Coco, ikiwa ni utunzaji wa Mazingira katika jamii inayowazunguka katika mradi wa Reli hiyo.

Akizungumza na waandishi wa Habari jioni ya leo, Mratibu wa Mazingira wa Kampuni hiyo Evodiaglory Mrengo amesema kuwa katika Ujenzi wa Reli wanatambua umuhimu wa utunzaji wa Mazingira katika kujenga afya salama kwa jamii wanayoizunguka katika miradi.

Amesema kuwa kufanya usafi  Ufukwe wa Coco ni mojawapo ya kazi za kijamii na Mazingira,na kwama kila Kampuni ikipata muda wa kufanya kazi ya kijamii ni vyema ikafavya hivyo.Mrengo amesema kuwa kufanya usafi ni kuhamasisha Wafanyakazi na jamii ya Mkoa wa Dar es Salaam kuwa mstari wa mbele katika utunzaji na uhifadhi wa fukwe za bahari ikiwa ni sehemu muhimu za mapumuziko.

Mjumbe wa Serikali ya Mtaa na Mwenyekiti wa Kamati ya Mazingira Oysterbay Peter Mushi amesema wanatambua mchango wa Kampuni ya Yapi Merkezi kufanya usafi katika ufukwe wa Coco.
 Wafanyakazi wa Yapi Markezi wakiweka Takataka katika mifuko walivyofanya usafi katika ufukwe wa Coco, leo jijini Dar es Salaam.
 Kiongozi Mkuu wa Afya na Mazingira wa Kampuni ya Yapi Markezi Erdem Yuksel akizungumza  kuhusiana na Kampuni hiyo kutoa mchango katika maeneo mbalimbali ikiwemo kufanya usafi katika ufukwe wa Coco leo  jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay na Mwenyekiti wa Kamati ya Mazingira wa Mtaa huo Peter Mushi akizungumza kuhusiana na Ujio wa Kampuni ya Yapi Markezi kufanya usafi katika ufukwe wa Coco,jijini Dar es Salaam.
 Mratibu wa Mazingira wa Kampuni ya Yapi Markezi Evodiaglory Mrengo akizungumza na waandishi habari kuhusiana na usafi wa Kampuni hiyo waliofanya katika Ufukwe wa Coco ,jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Ujenzi wa Reli ya Kisasa Yapi Markezi wakifanya usafi katika ufukwe wa Coco ikiwa ni kutoa msaada kwa jamii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...