Na Felix Mwagara, MOHA-Ngara.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema baadhi ya viongozi wa dini nchini wamejipenyeza na kuanzisha makanisa na misikiti kwa lengo la kuanzisha vichaka vya kujificha ili tujue ni watu wa Mungu kumbe wanataka kufanya uchochezi na kuvuruga amani nchini.
Lugola amesema Serikali ya Rais Dkt. John Magufuli haitawavumilia wale wote walioanzisha taasisi hizo kwa lengo lao binafsi na itahakikisha inawashughulikia ipasavyo bila kuwaonea huruma.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia ya wananchi wa Mji wa Ngara, leo, Lugola amesema makanisa na misikiti ambayo imesajiliwa na Wizara yake hatakubali kuona viongozi hao ambao wanajifanya kuwa na watu wa Mungu kumbe wanamalengo hayo binafsi.
“Makanisa na miskiti itakayobainika ina malengo hayo, sitaona haya kuifutia usajili, na pia nawataka viongozi wa dini endapo migogoro inaibuka hakikisheni mnaitatua wenyewe kwa amani,” alisema Lugola.
Lugola ameongeza kuwa, Serikali inaheshimu imani ya dini na pia viongozi wao wanamchango mkubwa katika maendeleo ya nchi kutokakana na maombi pamoja na kuwaongoza waumini wao vizuri, lakini pia wapo baadhi ya viongozi hao wa dini, wanaingiza masuala ya siasa makanisani na misikitini.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na wananchi wa Mji
wa Ngara, Mkoani Kagera (hawapo pichani), katika Mkutano wa hadhara
uliofanyika mjini humo, leo. Katika mkutano huo, Lugola amesema baadhi
ya viongozi wa dini nchini wamejipenyeza na kuanzisha makanisa na
misikiti kwa lengo la kuanzisha vichaka vya kujificha ili tujue ni watu
wa Mungu kumbe wanataka kufanya uchochezi na kuvuruga amani nchini.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Askari na
Watumishi wa Wizara yake wa Wilaya ya Ngara, Mkoani Kagera (hawapo
pichani), katika kikao hicho, Lugola aliwataka watumishi hao wafanye
kazi kwa kujituma bila kuchukua rushwa. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya
Ngara, Luten Kanali Michael Mtenjele. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Kagera, Revocatus Malimi.
Baadhi
ya Askari na Watumishi wa Mjini Ngara, Mkoani Kagera wakimsikiliza
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (hayupo pichani) wakati
alipokua anajibu maswali ya watumishi hao kuhusu masuala mbalimbali ya
Wizara yake, katika kikao kilichofanyika mjini humo, leo. Picha zote na
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...