Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (wa pili kushoto aliyevaa suti) akipewa maelezo na wafanyakazi wa kivuko cha MV. MKONGO mara baada ya kukagua kivuko hicho. Kivuko cha MV. MKONGO kinatoa huduma katika mto Rufiji kati ya Mkongo na Utete wilayani Rufiji mkoani Pwani na kina uwezo wa kubeba abiria 40 kwa wakati mmoja.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua mashine ya kupimia uwiano wa tairi za magari katika karakana ya TEMESA mkoa wa Manyara wakati wa ziara yake mkoani humo. Kushoto ni Meneja wa Temesa mkoani Manyara Mhandisi Margreth Julian.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (wa pili kushoto) akishuka kutoka kwenye kivuko cha MV. MALAGARASI mara baada ya kumaliza kukagua utendaji kazi na hali ya usalama wa kivuko hicho kinachotoa huduma katika mto Malagarasi kati ya Ilagala na Kajeje mkoani Kigoma, kivuko hicho kina uwezo wa kubeba abiria 100 na magari 6 sawa na tani 50. Wa kwanza Kushoto ni Nahodha wa kivuko Kassimu Mkitege. 
Abiria wakiingia katika kivuko cha MV. MALAGARASI tayari kuanza safari kutokea upande wa Ilagala kuelekea upande wa Kajeje, kivuko cha MV MALAGARASI kinatoa huduma katika mto Malagarasi kati ya Ilagala na Kajeje mkoani Kigoma na kina uwezo wa kubeba abiria 100 na magari 6 sawa na tani 50. 
Kivuko cha MV. MALAGARASI kikielea katika mto Malagarasi, kivuko hicho cha tani 50 kina uwezo wa kubeba abiria 100 na magari 6 kwa wakati mmoja na kinatoa huduma kati ya Ilagala na Kajeje mkoani Kigoma.
Nahodha wa Kivuko cha MV. MALAGARASI Kassimu Mkitege kushoto akiwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Maselle kulia wakati alipokua akikagua hali ya usalama na utendaji kazi wa kivuko hicho. Kivuko cha MV MALAGARASI kinatoa huduma katika mto Malagarasi kati ya Ilagala na Kajeje mkoani Kigoma. 

PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO - (TEMESA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...